Wenyeviti wa Serikali za Mtaa wa CUF wamuunga mkono Profesa Lipumba
Wenyeviti
 50 wa Serikali za Mitaa  wa CUF Mkoa wa Dar es Salaam wametangaza 
kuunga mkono uamuzi wa Baraza Kuu la Uongozi la CUF la upande wa 
Mwenyekiti wa CUF anayetambuliwa na Msajili wa Vyama vya Siasa, Profesa 
Ibrahim Lipumba kuwa vua uanachama wabunge  wanne wa viti maalumu na 
madiwani wawili.
Wabunge
 waliovuliwa uanachama ni  Halima Ali Mohamed, Khadija Salum Ally,  
Salma Mohamed Mwasa, Miza Bakari Haji, Raisa Abdallah Mussa, Riziki 
Shahari Mngwali, Saumu Heri Sakala na Severina Mwijage.
Wakiwakilisha
 wenzao 36 wenyeviti 14 kutoka mitaa mbalimbali ya halmashauri za 
manispaa tano  za Dar es Salaam wamesema wamefikia hatua hiyo baada ya 
kuridhisha na kazi nzuri inayofanywa na Profesa Lipumba.
Akizungumza
 kwa niaba ya wenzake 14 mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Keko Mwanga 
B, Shilingi Shilingi amewaambia wanahabari  leo Jumanne Agosti 8 
wanaunga mkono uamuzi wote wa Baraza Kuu la Uongozi kwa kuwa wabunge hao
 wamebainika kukihujumu chama hicho.
"Tunamtambua
 Maalim Seif Sharif Hamad kama katibu mkuu lakini kwa sasa nafasi yake 
inakaimiwa na Magadalena Sakaya kutoka na yeye kushindwa kutekeleza 
majukumu yake kwa mujibu wa Katiba ya CUF," amesema Shilingi
Mbali
 na hilo Shilingi amewataka watu wanaoingilia mgogoro wa chama hicho 
kuacha mara moja na kwamba mgogoro ni wa kikatiba na suala hilo lipo 
mahakamani muda si mrefu uamuzi utatolewa.
 

 
 
 
 
