Mafuta yaadimika Tarime baada ya vituo vitano vya kuuzia mafuta kufungwa sasa lita yauzwa sh 3000




Waitara Meng'anyi.

Shirika la Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) limefunga vituo saba vinavyotoa huduma kwa magari mjini  kwa kutoa huduma ya luuza mafuta bila kuwa na mashine za kutolea risti za (EFD).

Vituo hivyo viwili ni vya kampuni ya  Efco inayomilikiwa na mbunge wa Musoma Mjini Vedustus Mathayo, viwili vya mfanyabiashara maalufu wilayani hapa Peter Zakaria kimoja Nyamongo na Viwili vya Mairo.

Meneja TRA  mkoa wa Mara Ernest Nkang'aza alisema vituo vyote ambavyo havina mashine za EFD vitaendelea kufungwa hadi hapo vitakapotekeleza agizo hilo.

"Hili ni zoezi la nchi nzima kwa vituo vyoye visivyokuwa na mashine za elektroniki ya kutolea risti za malipo havitatoa huduma hiyo hadi hapo vitakapoyimiza agizo hilo," alisema Nkang'aza.

Pia amewatahadhalisha wamiliki wa vyombo vya moto kutokujiaminisha kupata huduma ya mafuta nchi jirani ya kenya kwani wanakiuka  sheria.

"Kuingia nchi jirani na kunywesha mafuta magari yao ni kinyume cha sheria hivyo idara ya uhamiaji wanalifuatilia suala hilo kuwa baini wanaofanya kazi hiyo," alisema.

Zoezi hilo la kufunga vituo hivyo lilitekelezwa jana mchana majira ya saa nane, hatua ambayo imesababisha ukosefu wa mafuta na kusababisha kupanda kwa nauli mara mbili ya nauli ya kawaida.

Wakizungumza na CLEO24NEWS  wamiliki wa magari na madereva walisema kuwa imewalazimu kwenda kutafuta nishati hiyo nchi jirani ya Kenya.

Mwita Mseti anayefanya safari zake Tarime Musoma alisema kuwa ilimzamu kuwenda kutafuta nishati hiyo mpakani Sirari ambapo ni umbali wa kilomita 18 kutoka mjini Tarime ambapo kwa sasa mafuta yanapatikana.

"Upatikanaji wa mafuta kwa saa hili moja umekuwa shida kweli, hatujui hapo kesho hali itakuwaje kwani mahitaji yatakuwa makubwa zaidi," alisema Mseti.

Aidha mtumia usafari wa pikipiki Amina Abdalla mkazi wa mtaa wa Rebu senta alisema kuwa gharama nauli imepanda maradufu kuliko ilivyokuwa saa chache  zilizopita baada ya kufungwa kwa vituo vyote saba.

"Pale tulipokuwa tunalipa 1000 imepanda hadi 2000, ukihoji wanadai wanafuata mafuta Sirari," alisema Abdalla.

Muuzaji wa rejareja wa  mafuta ya peterol Dickson Daudi alisema kwa sasa lita moja ni sh,3000 .

"Nilikuwa na akiba nyumbani na hapa ndipo ninapata faida kwani leo asubuhi (jana) nilikuwa nauza sh,2500 kwa lita lakini kuanzia saa nane tumepandisha bei kuwa sh3000 na hali ikiendelea hivi kesho tutauza sh 4000 kwa lita," alisema Daudi.
Powered by Blogger.