REA AWAMU YA TATU YAZINDULIWA SIMIYU, VIJIJI 347 KUPATA UMEME



Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Mhe.Dkt.Medard Kalemani (mwenye suti nyeusi katikati) akikata utepe kabla ya kuzindua Mradi wa Umeme Vijijini (REA) Awamu ya Tatu Mkoani Simiyu katika Kijiji cha Nangale wilaya ya Itilima

Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Mhe.Dkt.Medard Kalemani akizindua Mradi wa Umeme Vijijini (REA)Awamu ya Tatu Mkoani Simiyu katika Kijiji cha Nangale wilayani Itilima (kushoto) Mkuu wa mkoa huo, Mhe.Anthony Mtaka.
Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Mhe.Dkt.Medard Kalemani akizungumza na wanachi wa Wilaya ya Itilima wakati wa Uzinduzi waMradi wa Umeme Vijijini (REA) Awamu ya Tatu  Mkoani Simiyu uliofanyika  katika Kijiji cha Nangale wilaya ya Itilima.
Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Mhe.Medard Kalemani akiwaonesha wananchi Kifaa kiitwacho UMETA(Umeme Tayari) ambacho hutumika kuleta nishati ya umeme katika nyumba ambazo haziwezi husukwa nyaya wakati wa uzinduzi wa Mradi wa Umeme Vijijini (REA) Awamu ya Tatu  Mkoani Simiyu katika Kijiji cha Nangale wilaya ya Itilima
Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Mhe.Dkt.Medard Kalemani( wa pili kulia) pamoja na baadhi ya viongozi wa mkoa wa Simiyu wakicheza kuelekea kuwatuza wasanii waliokuwa wakitoa burudani (hawapo pichani) wakati wa uzinduzi wa Mradi wa Umeme Vijijini (REA)Awamu ya Tatu Mkoani Simiyu uliofanyika katika Kijiji cha Nangale wilaya ya Itilima.
Baadhi ya wananchi wa Wilaya ya Itilima wakimsikiliza Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Mhe.Dkt.Medard Kalemani(hayupo pichani) wakati wa wakati wa uzinduzi wa Mradi wa Umeme Vijijini (REA)Awamu ya Tatu Mkoani Simiyu katika Kijiji cha Nangale wilaya ya Itilima.



Jumla ya Vijiji 347 Mkoani Simiyu vinatarajia kupata Umeme kupitia Mradi wa Umeme Vijijini (REA) awamu ya Tatu ambao utatekelezwa katika kipindi cha miezi 24 kuanzia mwezi Julai 2017.

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Mhe.Dkt.Medard Kalemani wakati wa Uzinduzi wa Mradi wa Umeme Vijijini (REA) Awamu ya Tatu na utambulisho wa Mkandarasi wa mradi katika Kijiji cha Nangale, Kata ya Ndolelezi Wilaya ya Itilima Mkoani Simiyu.

“Mradi wa REA awamu ya tatu utapeleka Umeme katika vijiji vyote vya Mkoa wa Simiyu hilo la kwanza, pili mradi huu utapeleka Umeme katika vitongoji vyote hata vijiji ambavyo vilipelekewa Umeme lakini baadhi ya vitongoji vyake bado havina, katika awamu hii navyo vinapelekewa” amesema Kalemani. 

Ameongeza kuwa Umeme wa REA awamu ya tatu pamoja na kuwanufaisha wananchi katika makazi yao kwenye vijiji vyote 347 vilivyosalia pia utapelekwa katika Taasisi za Umma zikiwepo shule, vituo vya kutolea huduma za afya, visima na mitambo ya miradi ya maji pamoja na nyumba za ibada( makanisa na misikiti).


Akimkabidhi Mkandarasi wa Mradi wa REA Awamu ya Tatu ambaye ni Kampuni ya JV White City International kwa Wananchi wa Mkoa wa Simiyu, Dkt.Kalemani amemtaka  kuhakisha kuwa anatekeleza mradi  ndani ya muda uliopangwa (miezi 24), akiwatumia wakandarasi wasaidizi wenye sifa kutoka ndani ya mkoa na kuwapa ujira wao kama inavyotakiwa pamoja na  kununua vifaa vyote zikiwemo nguzo na transifoma hapa nchini.


Amemtaka Meneja wa TANESCO Mkoa wa Simiyu, Mhandisi Rehema Mashinji kusimamia na kuhakikisha kuwa wakandarasi watakaowaunganishia wananchi Umeme ni wale walioidhinishwa na shirika hilo ili kuepuka Vishoka ambao watawaongezea wananchi gharama zisizo za lazima.
HABARI NA PICHA NA COSTANTINE MATHIAS SIMIYU
Powered by Blogger.