TASAF YASIKITISHWA NA WALENGWA KUTOTIMZA MASHARTI.

Mmoja wa wanufaika wa TASAF III katika Kijiji cha Migato akipokea fedha katika zoezi la uhawilishaji lililofanyika kijijini hapo jana.

Mkurugenzi wa Ukaguzi wa Ndani kutoka TASAF Makao Makuu, Ndg. Christopher Sanga (wa pili kulia) akizungumza na wanufaika wa TASAF III katika kijiji cha Migato wilaya ya Itilima kuhusu kutimiza masharti ya ruzuku toka TASAF
. Ndg. Wolter Soer kutoka Benki ya Dunia (wa kwanza kushoto) na Mkurugenzi wa Ukaguzi wa Ndani kutoka TASAF Makao Makuu, Ndg. Christopher Sanga(mwenye miwani) wakimsikiliza mmoja wa wanufaika wa TASAF III katika Kijiji cha Migato akiwaeleza juu faida anazopata kupitia fedha anazopokea kupitia mpango huo.

Baadhi ya wanufaika wa TASAF III wa Kijiji cha Migato wakiimba wimbo maalum wa kuwakaribisha wataalam kutoka TASAF Makao Makuu, Benki ya Dunia na wadau wengine wa maendeleo (wadau washiriki wa mradi) ambao ni UNDP, UNFPA, ILO na Umoja wa Nchi za Ulaya(EU) waliofika kufanya tathmini ya utekelezaji wa mradi wa TASAF III Wilayani Itilima mkoani Simiyu




Na COSTANTINE MATHIAS, Simiyu


MFUKO wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) umesikitishwa na kitendo cha wanufaika kutotimiza masharti ya mpango huo hali inayosababisha kukosa fedha katika ruzuku hiyo kwa kaya maskini.


Hayo yalibainishwa jana na Mkurugenzi wa Ukaguzi wa ndani kutoka makao makuu  (TASAF) Christopher Sanga alipotembelea wanufaika katika kijiji cha Migato wilayani Itilima mkoani Simiyu na kusema kuwa lengo la serikali kuwanufaisha ni kuwakwamua kimaisha.


Alisema kuwa serikali inatoa fedha hizo kupitia ruzuku ya masharti ili watoto waweze kupata mahitaji yao ya kila siku ikiwemo huduma ya elimu na matibabu kwa kupelekwa kliniki.


Sanga aliwataka wazazi kuwapa nafasi ya kwenda shule watoto ili kutimiza masharti ya mpango huo ana pia waweze kufikia malengo ya serikali ya kunusuru familia zao.


‘’mnaonekana kurudisha nyuma jitihada za serikali ambazo lengo lake ni kuwaondoa katika hali mliyokuwa nayo awali ya umasikini na kupiga hatua kimaisha katika kukidhi mahitajia ya kila siku’’ alisema Sanga.


Aliongeza kuwa changamoto ya kutotimiza masharti kwa wanufaika hao bado ni tatizo hali inayosababisha kaya kupoteza ruzuku yake na kupungua kwa malipo ya wanufaika.


Alisema kuwa Lengo la serikali ni kujenga nguvukazi  ya watu wake katika kutatua kero za wananchi na mtoto asipopelekwa kliniki akiwa mdogo, uzalishaji utapungua akiwa mkubwa.


Nao baadhi ya wanufaika wa mpango huo walikiri kuwepo kwa baadhi ya familia kutotimiza masharti ya ruzuku hizo na kusababisha fedha kurudishwa TASAF makao makuu.


‘’kuna baadhi ya familia watoto hawafiki shuleni, lakini asubuhi wanaaga na kuvaa sare kwenda shule…hivyo ni jukumu la kila mzazi kuhakikisha mtoto wake anahudhuria masomo ili aweze kutimiza masharti ya mpango huu’’ alisema Minza Bulayi Mkazi wa Migato.


Katika kipindi cha mwezi Novemba hadi Disemba kaya 29 kati ya 99 kijijini hapo hazikuchukua ruzuku kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo walengwa kushindwa kutimiza masharti ya Elimu na Afya kwa lengo la kuwa na jamii yenye afya na elimu bora kwa watoto.
 



Powered by Blogger.