SHIRIKISHO LA VYAMA VYA WACHIMBAJI WADOGO WA MADINI TANZANIA WAMPA TANO RAIS MAGUFULI UAMUZI KUHUSU MCHANGA WENYE MADINI
Shirikisho la Vyama vya Wachimbaji Wadogo wa Madini Tanzania (FEMATA)
limempongeza mheshimiwa rais John Pombe Magufuli kwa hatua
alizozochukua baada ya kupokea ripoti ya uchunguzi wa mchanga wenye
madini ambapo miongoni mwa maamuzi yaliyochukuliwa na rais ni kusitisha
usafirishaji wa mchanga huo nje ya nchi.
Pongezi hizo zimetolewa leo na rais wa shirikisho hilo John Bena wakati
akiongea na waandishi wa habari na viongozi mbalimbali wa wachimbaji
wadogo wa madini.
Bena amesema uamuzi uliochukuliwa na rais Magufuli utasaidia nchi
kupata faida kwa madini ambayo yalikuwa yakichukuliwa bila kufahamu
kuwa kuna madini mengine ndani yake.
Kwa upande wake mtendaji mkuu wa FEMATA Haroun Kinega akiwataka
wachimbaji wadogo kuunga mkono juhudi za mheshimiwa rais Magufuli.
Naye Mwenyekiti wa Chama Cha Wachimbaji Madini mkoa wa Singida Robert
Marando amesema hatua alizo chukua rais Magufuli zitawasaidia
wachimbaji wadogo kupata faida,kwani walikuwa wakishafirisha shaba nje
ya nchi huku ikiwa na madini mengine.
Imeandaliwa na Raymond Herman wa Malunde1 blog