Riziki Rulida atoa agizo hili kwa Maaskofu
Mbunge Viti Maalum kupitia Chama Cha Wananchi (CUF), Mhe. Riziki Rulida amewataka Maaskofu nchini wasijiingize katika masuala ya siasa kwa sababu siasa ni propaganda, badala yake waendelee kueneza neno la Mungu na kuwahimiza Waumini kutenda matendo mema.
Riziki amesema hayo Bungeni Mjini Dodoma leo alipopata nafasi ya kuzungumza ikiwa ni siku chache Tangu Baraza la Maaskofu wa KKKT watoe waraka wao unaozungumzia hali ya amani nchini. Amefafanua kwamba, kazi ya Maaskofu ni kusimamia dini na waumini wake wala si kufanya saiasa.