Graca Machel awataka vijana kuwa na mipango ya maendeleo

Aliyekuwa mke wa rais wa Msumbiji, Samora Machel, Mama Graca Machel  ambaye pia ni mwanzilishi wa Taasis ya Graca Machel Trust amewataka vijana kuweka mipango ya kujiletea mandeleo ya kiuchumi .
Mama Machel alisisitiza hayo Jumatano wiki hii alipokuwa akizungumza  na vijana wa nchi mbalimbali  jijini Dar es salaam katika mjadala uliofanyika kujadili changamoto zinazowakabili vijana wa Afrika katika hasa katika eneo la uchumi.

Mjadala huo ulikuwa ni sehemu ya maandalizi ya vijana duniani ambayo imeadhimishwa leo Agosti 12 .

 Graca Machel  ambaye pia  aliyekuwa mke wa rais wa kwanza wa  Afrika Kusini, Nelson aliwataka vijana kuacha kulalamika na baadala wawe wabunifu.

Powered by Blogger.