ASKARI WA KENYA AKATWA KIGANJA CHA MKONO WA KULIA WATU WATATU RAIA WA KE...





KAMANDA WA POLISI TARIME RORYA SACP HENRY MWAIBAMBE AKIONGEA NA VYOMBO VYA HABARI







Kamanda wa
pilisi MKoa wa Polisi Tarime Rorya SACP Henry Mwaibambe  akiongea na Waandishi wa Habari kuhusu tukio
la Inspekta James Mnuve 46 raia na Askari wa Kenya na Mkazi wa Tanariver
aliyejeruhiwa kwa kukatwa kiganja cha mkono 
wa kulia na kudondoka chini pamoja na kujeruhiwa sikio la kulia na
kusababishiwa ulemavu wa kudumu amesema kuwa mpaka sasa watu watatu raia wa Nchi jirani ya Kenya
ambao ni Anjeli Wanja Prisca Mwita Swagi28 Mfanyabiashara, Daneil Andrew
  Onchari25 na Michael Malindi Omahe wote wakazi wa Sirare Isbania Nchini
Kenya wanashikiliwa na jeshi la polisi na watafikishwa mahakamani baada ya mahojiano.





Tukio hilo
lilitokea Mnamo julai 13 Mwaka huu katika Mtaa wa Msati Kata ya Nkende
Halmashauri ya Mji wa Tarime Mkoani Mara.





Hata hivyo Kamanda
ameongeaza kuwa Jeshi la Polisi 
linaendelea kumtafuta mtuhumiwa aliyejulikana kwa jina la Gekayi Chacha
Mkazi wa kijiji cha Soroneta ambae anatuhumiwa kwa kosa la  kujeruhi mtu aitwaye Ryoba Nyamhanga23 Mkazi
wa kijiji cha Soroneta ambaye alijeruhiwa kwa kukatwa panga Shingoni,Upande wa
kushoto mwa bega na Mgongoni  amelazwa
Hospitali  ya wilaya ya Tarime na hali
yake ni mbaya.

SIKILIZA
KAMANDA WA POLIS AKIZUNGUMZIA MATUKIO HAYO.


Powered by Blogger.