Ujumbe wa Hussein Bashe kwa Waziri Nape baada ya ripoti kumuhusu Makonda

March 22, 2017 Waziri wa habari, utamaduni, sanaa na michezo Nape Nnauye alikabidhiwa ripoti na kamati aliyoiunda kwa ajili ya kuchunguza tukio la tuhuma za uvamizi alioufanya Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda katika ofisi za Clouds Media Group usiku akiwa na Askari wenye silaha.

Waziri Nape baada ya kupokea ripoti hiyo aliongea na Waandishi wa habari kueleza kuwa hatua inayofuata ni yeye kuiwasilisha ripoti hiyo katika ngazi kuu ya uongozi akiwemo Rais Magufuli ili hatua stahiki iweze kuchukuliwa.

 

Baadhi ya walioonesha kuipokea taarifa za ripoti hiyo ni pamoja na Mbunge wa Nzega mjini Hussein Bashe ambaye akaamua kuandika ujumbe kupitia account yake ya Twitter huku akipongeza hatua ya Waziri Nape.

Powered by Blogger.