NDOA FEKI ZAFIKA TARIME, WANAUME SASA WAPORWA MALI NA WAKE ZAO.



Kutokana na kuporomoka kwa maadili katika jamii ndoa bandia zimeibuka kwa wanawake kuolewa na wanaume wenye mali kisha kuvunja ndoa baada ya muda mfupi na kudai kugawana mali hiyo.

Mwenyekiti wa serikali ya mtaa wa Nkende shuleni wilayani Tarime mkoani Mara Samwel Kisege amesema katika mtaa wake ameamua kesi nane kwa muda wa uongozi wake  na kuwa anakerwa na kitendo cha wananwake wanaolewa na kuvunja ndoa zao kwa muda mfupi kwa lengo la kupata mgawanyo wa mali huku yeye akisema hii ni njia mpya ya utafutaji mali kwa wanawake.

“Sasa ninaomba nyie waandishi mtusaidie jinsi ya kuanzisha chama cha wanaume ili kudai haki zetu kwa wanawake hawa, maana tunadhalilika sasa, unatafuta mali mwenyewe lakini ukioa unaanza kupata shida na wakati mwingine hata nyumba uliyojenga unashindwa kuishi ndani yake,’alisema Kisege.

Kwa kipindi cha mwaka mmoja na nusu niliokuwa mwenyekiti wa mtaa wa Nkende amekutana na kesi zaidi ya nne  imekuwa ni kama mchezo unaofanyika wa kuvunja ndoa wanawake wanaolewa na mwanaume mwingine ikiwa lengo lao nikujitafutia mali kwa njia hiyo.

“wanaovunja ndoa ni wenye uzazi wa watoto wawili au mmoja, kisha huolewa kwingine, imefikia wakati kwa wanawake huwanyima hata tendo la ndoa waume zao,”alisema Kisege.

Pia inaonyesha kuwa kuwepo kwa tabia hizi ni kutokana na wazazi kushindwa kudhibiti maadili ya watoto wao ambapo wengi wamekuwa wakijichukulia maamzi wenyewe bila kuwashirikisha wazazi wakati mwingine wakati wa kuolewa.

Kitendo hicho kimeonekana kuwa kibaya kwa wanaume na jamii nzima kwani kinarudisha nyuma malengo ya mtu kwa kuwa humfanya mwanaume kuanza maisha upya baada ya mgawanyo wa mali ambapo zamani kwa kabila la Wakurya haikuwepo tabia hiyo.

Joseph Malele  ni mmoja ya wawanaume walionja mkasa huu  alisema hamuna wanawake hao  kwani wengi wao wanahitaji mali wakati mnakubaliana kuona kutokana na maisha kuwa  magumu ndio maana wanafanya hivyo.

“Mambo yamekuwa ni magumu kwetu wanaume kwa kuwa wanadai kuwa haki sawa, tofauti na ilivyokuwa zamani ambapo wanaume walikuwa na sauti ya kukataa,”alisema Malele

Aidha mkazi wa mtaa wa Sabasaba mjini Tarini Helena Peter yeye alisema kuwa ni baadhi ya wanawake ndio wamekuwa wakitaka kugawana mali lakini wengi wao wamekuwa wakiishi vizuri na wanaume zao.

“Siyo wote wanang’ang’ana na kuomba mali ili wagawane mali, lakini kama nikiona mwanaume anataka kuoa mke mwingine lazima tugawane mali, lakini siyo vizuri kutumia njia hii kujipatia mali ya mume wako,”alisema Peter.


Powered by Blogger.