ZAIDI YA WAUMINI WAPYA 500 WABATIZWA MKOANI MARA



ZAIDI ya waumini wapya 500 wamemkubali Yesu kuwa Bwana na Mwokozi wao kwa kuzamishwa ndani ya maji mengi katika kanisa la Waadventista Wasabato  katika Konferensi ya Mara.

Idadi hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa Konferensi ya Mara Mchungaji George Ojwang Ezekiel wilayani Tarime wakati alipofanya mahojiano na mwandishi wa blog hii  wakati akikagua Zahanati ya Tarime iliyoko katika kanisa la Turwa mtaa wa Turwa Mjini Tarime.

Mchungaji Ojwang amesema kuwa idadi hiyo imetokana na mahubiri ya Total Membership Involvement (TMI) yanayoendeshwa kwenyen vituo 350 mkoa mzima wa Mara.

Amesema kuwa kupitia vituo hivyo ambavyo vimeungamishwa na mahubiri ya Ushindi Hatimaye yanayorushwa Mubashara kutoka kanisa la Mabatini Jijini Mwanza, waumini wapya zaidi ya 500 wamemkubali Yesu kuwa Bwana na mwokozi wa Maisha yao na kubatizwa.

"Tulitarajia kuwa na vituo 417 kama ilivyo idadi ya makanisa Mara Konferensi lakini kutokana na hali ya uchumi baadhi ya makanisa yameshindwa kupata vifaa vya kuendeshea vituo vyao," amesema Mwenyekiti wa kanisa Mara Konferensi Mchungaji Ojwang.

Aidha katika hatua nyingine mchungaji Ojwang akiambatana na katibu mkuu wa konferensi hiyo Mchungaji Enock Sando, mkurugenzi wa Mawasiliano,  mchungaji Joseph Matongo, mkurugenzi wa Idara ya afya na mhazini wa jimbo hilo amefungua kituo cha afya Bukwe kilichoko Wilayani Rorya baada ya kusimama kutoa  Huduma kwa kipindi cha mwaka mmoja huku akifanya ukaguzi katika zahanati ya Tarime iliyoko katika kanisa la Turwa mjini Tarime.

"Kuanzia Leo kituo cha afya Bukwe kimefunguliwa rasmi ili kianze kutoka Huduma kwa wagonjwa, nitumie fursa hii kuwataarifa wananchi na wakazi wa Tarime na Rorya kwenda kupata Huduma ya matibabu katika vituo vyetu vilivyo karibu nao maana siyo kuwa tunatoa Huduma za kitabibu tu Bali waganga huomba kabla ya kutoa Huduma," alibainisha.

Kituo cha afya Bukwe kilifungwa baada ya kuonekana kuwa na mapungufu kadha wa kadha na kuulazimu uongozi kukifunga ili kukiweka katika mazingira mazuri ya utoaji Huduma kwa wagonjwa jambo ambalo sasa limetekelezwa kwa kiwango kinachostahili.

Aidha amewataka wachungaji wa mitaa, wazee wa makanisa na wakurugenzi makanisani kuhudhuria mkutano wa GAiN Mara konferensi utakaofanyika mwishoni mwa mwezi huu katika kanisa la Tarime kati Wilayani Tarime kwa muda wa siku tano.

"Viongozi hawa wakihudhuria mkutano huu utawajengea uwezo wa kuenenda na wakati katika kutoa utume wetu tulioitiwa, na wasipange kukosa mikutano hiyo," alisema Mchungaji Ojwang.



Powered by Blogger.