Serikali Kutowavumilia Wanaojihusisha na Ukeketaji.
NA
HASSAN SILAYO
Katibu
Mkuu Wizara ya Afya Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii Bi.Sihaba Nkinga amekemea
vitendo vya Ukeketaji kwa watoto nchini na kuahidi kuwachukulia hatua kali za
kisheria wale watakaobainika.
Akiongea
wakati wa Mahafali ya watoto 46 waliokimbia kukeketwa na kujiunga na Kituo cha
kulea watoto hao cha ATFGM Kilichopo Masanga Tarime Vijijini Bi.Sihaba alisema
kuwa suala la ukeketaji ni kinyume na sheria za nchi na haki za binadamu na ni suala lenye madhara kwa maisha ya
watoto.
“Hatukubaliani
na suala hili kwani linarudisha maendeleo ya nchi yetu,suala hili pia
linachangia kurudisha fikra za vijana wetu na kubatilisha ndoto za vijana wetu,
tunao muda wa kujirekebisha na kama tulikuwa tunaendelea basi turudi nyuma”Alisema
Bi. Sihaba.
Bi.
Sihaba amesema kuwa jamii inayo wajibu wa kulinda na kuendeleza mila zenye
kuleta maendeleo na kuacha kulinda na kukumbatia mila zinathoathiri maisha ya
binadamu kwani sio suala sahihi kwani mila nyingine zinagharimu maisha ya
vijana wetu.
Akizungumza
katika mahafali hayo Mkuu wa Wilaya ya Tarime Bw. Glorious Luoga amewakemea
wazazi watakaothubutu kuwakeketa wasichana wanaotoka katika kituo hicho baada
ya mafunzo na wale watakao watakaowatahiri watoto wa kiume kwa mara ya pili
baada ya kufanyiwa tohara salama hospitalini.
“Niwaeleze
wazazi na walezi, wapo wanaowalazimisha kuwafanyia tohara ya pili watoto wa
kiume baada ya kufanyiwa tohara salama, atakayegundulika kufanya tukio hilo
tutamshughulikia kwa kumchukulia hatua kali za kisheria ili aone uchungu
anaoupata mtoto wakati wanawatahiri kwa mara ya Pili” Alisema Bw. Luoga.
Naye
Mkuu wa Wilaya ya Bunda Bi. Lydia Bupilipili amewasihi wazazi kuacha tabia ya
ukeketaji na kuwapeleka watoto shule ili waweze kutimiza malengo yao kwani kila
mtoto ana talanta aliyopangiwa na mungu hivyo kufanya hivyo kuwakeketa na
kuwazuia kwenda shule ni kukatisha malengo yao.
Mkurugenzi
wa Kituo cha Kulea Watoto waliokimbia Kukeketwa cha (ATFGM-Massanga) Sister
Stella Mgaya ameshukuru juhudi zinazoendelea kuchukuliwa na uongozi wa wilaya
ya Tarime kukabiliana na tatizo hilo na kuendelea kuomba wadau kujitokeza
kuwaendeleza watoto wanaohitimu kituoni hapo.
“Tunashukuru
jitihada za Wilaya ya Tarime wamekuwa nasi bega kwa bega ila tunaomba wadau
wengine ikiwemo serikali kwani baada ya mafunzo watoto hawa wamekuwa wakitengwa
na familia zao na kuacha kuwapa mahitaji ya msingi hivyo kulazimu kituo
kugharamia masomo japo sio kwa kiwango cha kuridhisha” Alisema Sister Mgaya.
Wakisoma
Risala kwa Mgeni Rasmi Muwakilishi wa wahitimu hao Magreth Daniel ameiomba
serikali kuendelea kuwasaidia hasa baada ya mafunzo na kuepuka kutengwa na
familia pia kuendelea kuwachukulia hatua za kisheria wazazi,walezi na mangariba
wanaojishughulisha na vitendo vya ukeketaji.
Kituo
Kituo cha Kulea Watoto waliokimbia Kukeketwa cha (ATFGM-Massanga) kwa mwaka
jana kimepokea watoto 300 kutoka katika maeneo ya Tarime,Rorya,Bunda, Loliondo
na baadhi kutoka nchi jirani ya Kenya.