Polisi Mara yapata ushindi wa 1-0 dhidi ya Polisi Dodoma
POLISI Mara imetamba nyumbani kwanza
kwa kupata ushindi wa bao 1-0 kuitandika Polisi Dodoma katika mchezo
uliofanyika jana jumamosi katika uwanja wa Karume mjini Musoma.
Bao pekee la Polisi Mara
lilipatikana kwa mkwaju wa penati katika dakika ya 37 kupitia kwa
mshambuliaji Kaisi Pastory aliyefunga bao hilo na kuwainua mashabiki kwenye
viti vyao.
Bao hilo lilidumu kwa muda wote wa
mcheo huo hadi dakika 90 zilipomalizika matokeo hayakuweza kubadilika na
kuibuka na ushindi wa bao 1-0.
Kocha mkuu wa Polisi Mara, Henry
Mkanwa akiwa amejawa furaha alisema ndio mwanzo wa kufanya vizuri baada ya
kufanya vibaya kwenye mechi zilizopita na zinazofuata makosa yaliyopo
atayarekebisha.
“Matokeo haya ni baada ya kufanyia
kazi makosa yaliyokuwepo kwnye kikosi, maana wakati nakipokea kilikuwa kibaya
sana hasa kwenye umaliziaji, kwa mechi zilizotangulia nilikuwa nikisoma kikosi
na kuona mapungufu,” alisema Mkanwa.
Alisema kuwa siri ya ushindi wao ni
uongozi kuanza kusikiliza matakwa ya timu na kuyatekeleza mahitaji yake kwa
wakati ambapo pia wacheaji wa kikosi hicho wamepata mwamko wa kujituma.
“Bado hawakufanya vizuri kama
nilivyotaka tulitakiwa kupata mabao mengi makosa ya umaliziaji nimeyaona na
nitayafanyia kazi ili kuimaisha kikosi zaidi,” alisema Mkanwa.
Alisema kuwa timu ya Polisi Dodoma
anaifahamu vizuri kwani alikuwa Kocha wake, ndiyo maana alitumia udhaifu wao
kupata ushindi.
“Mashabiki wetu wajue kuwa huu ni
mwanzo wa kuwapa furaha timu iko vizuri na imenza mwendo kulekea kufanya
vizurri kwenye mechi zinazofuata,” alisema Mkanwa.