TARIME United imeichapa Tarime
Warriors mabao 2-1 kwenye mchezo wa kupimana nguvu uliopigwa mwishoni mwa wiki
(jumamosi) katika uwanja wa Serengeti mjini hapa.
Tarime Warriors ndio walitangulia
kupata bao la kuongoza katika dakika ya 25 kupitia kwa Hamis Moshi na kuegeuza
upepo wa mchezo huo kuifanya Tarime United kushambulia kwa nguvu zote.
Mashabulizi hayo yalizaa matunda
dakika ya 39 kwa Godson Daudi kuipatia timu yake bao la kusawaisha na kuongeza
bao la pili na la ushindi katika dakika ya 82, dakika nane kabla ya mchezo huo
kumalizika.
Kocha wa Tarime Warriors William
Oremo alisema timu yake iko vizuri na vijana wako katika hali nzuri na matokeo
hayo ndiyo hali halisi ya mchezo nimeyapokea na kwenda kufanyia marekebisho
mapunufu niliyoyaona.
“Wenzetu wamepata nafasi wameitumia
vizuri na kufunga bao la usindi, lakini kikosi changu kiko imara na kinafanya
vizuri ukizingatia kuwa vijana wetu wako chini ya umri wa miaka 20 (U20),”
alisema Oremo.
Kwa upande wake, kocha wa Tarime
United Hamis Bakari alitanda kutokana na ushindi huo kuwa kikosi chake
kinauwezo mkubwa ndio maana kilipatta ushindi.
“Timu yangu umeiona iko vizuri ndio
maana tumetanguliwa kufungwa lakini tumesawazisha na kuongeza bao la ushindi,”
alisema Bakari.
Mwiso.
|