WAISLAMU WATAKIWA KUFANYA KAZI.

SHEIKH MKUU MKOA WA SHINYANGA SHEIKH ISMAIL MAKUSANYA AKIZINDUA RASMI MASHINE ZA KUSAGA KATIKA MSIKITI WA IJUMAA BAKWATA WILAYANI TARIME MKOANI MARA


WAKISHUDIA TUKIO LA UZINDUZI WA MASHINE TATU ZA KUSAGA
SHEIKH WA WILAYA YA TARIME SHEIKHABDULHAKIM MURISHO SOUD AKIELEZA JAMBO BAADA YA KUZINDULIWA RASMI KWA MASHINE TATU ZA KUSAGA


Waumini wa dini ya Kiislamu wametakiwa Kuendelea kuswali ikiwa ni pamoja na kufanya kazi za uzalishaji ili kujiletea maemndeleo kama maandikomatakatifu yanavyosema ikiwa ni pamoja na kuwa na mashikamano wa pamoja kwa lengo la kuwasaiadia watu wenye mahitaji, Wakiwemo Walemavu, Wajane pamoja na Yatima.

 

Akifungua Rasmi Mashine Tatu za Kusaga katika Msikiti Mkuu wa Ijumaa Wilayani Tarime Mkoani Mara Sheikh Mkuu kutoka Mkoa wa Shinyanga Ismail Habibu Makusanya alisema kuwa Waumini wa Kiislamu wanawajibu mkubwa  wa kendelea kuswali ikiwa ni pamoja na kufanya kazi za uzailishaji kama maandiko matakatifu yanavyosema.

 

Hata hivyo Sheikh huyo aliongeza kuwa dini ya kiislamu bado inaimia kufanya kazi pamoja na kufanya baishara kwa lengo la kujipatia riziki  hivy amezidi kuwasisitiza waumini wote kuendelea kufanya kazi kwa ajili ya kuijipatia kipato

Hizi mashine Tatu zaidi ya Millioni 20 siyo haba ni kazi kubwa mliyofanya na watu wengine wanapaswa kuiga mfano wa waumini wa kiislamu wilaya ya Tarime kwani ni waumini pekee waislamu wa ujasiriamli pamoja na uzalishaji.

 

Awali wakisoma Risla mbele ya Sheikh huyo walisema kuwa awalia  kamati ya IQRA EDUCATION FUND mnamo mwaka 2009 iliwezakununu kiwanja na ilipofika mwaka 2013 ikileta wazo la kujenga na kuweka mradi wa mashine tatu kutokana na nguvu za waislamu wa Tarime kwa asilimia99% ambapo ghalamaza ununuzi  wa kiwanja zilikuwa 7,000,000 pamoja na usajili wa kiwanja hicho, ujenzi kutoka msingi hadi jingo kukamilika limegahalimu 10,294,086 pamoja na Mradi wa amshine Mbili za kusaga na moja ya kukoboa  zimeghalimu shilingi 9,291,986 hivyo kufanya ghalama zote  toka mwanzo hadi sasa kufikia shilingi 26,576,072.


Powered by Blogger.