PICHA KATIKA MATUKIO: MVUA ZILIZOAMBATANA NA UPEPO MKALI ZILIVYOFANYA UHARIBIFU SHULE YA SEKONDARI KISUMWA WILAYANI RORYA

MWALIMU MKUU WA SHULE YA SEKONDARI KISUMWA ILIYOPO WILAYANI RORYA MKOANI MARA JOSHUA JOHN  AKIONESHA JINSI MAHABARA ZILIVYOBOMOLEWA NA MVUA ZILIZONYESHA KWA KUAMBATANA NA UPEPO MKALI JANUARY 28 MWAKA HUU


Mvua ambazo zinaendelea kunyesha zikiambatana na upepo mkali  katika Wilaya ya Rorya Mkoani Mara zinaendelea kusababisha madhala makunbwa ambapo katika shule ya Sekondari Kisumwa Mvua kubwa iliyonyesha Januari 28 mwaka huu imefanya uharibifu mkubwa uanaokadiliwa zaidi ya Millioni 120 ambapo Mahabara Mbili zilianguka zote na chumba kimoja kuezuliwa bati , Madarasa Mawili yameezuliwa bati na mbao zake huku madarasa matatu yakiezuliwa  upande mmoja hivyo Majengo Nane yamekumbwa na janga hilo ukiwemo uharibifu wa vifaa vya mahabara na na vifaa vya shule.

 Joshua John ni Mwalimu Mkuu katika shule ya Sekondari Kisumwa wilayani rorya Mkoani Mara amezidi kuiomba serikali kupitia kamati ya maafa wilaya kulifanyia kazi suala hilo ili kumaliza changamoto inayowakumba baada ya  madarasa kupungua na vifaa vya mahabara kuaribika .

Hata hivyo amezidi kuwaomba Wadau wa maendeleo kujitolea ili kusaidia shule hiyo kwani mali nyingi zimeaharibiwa vibaya.
MOJA YA MAHABARA ILIYOEZULIWA MABATI BAADA YA MVUA KALI LI ILIYOAMBATANA NA UPEPO KUNYESHA WILAYANI RORYA MKOANI MARA KATIKA SHULE YA SEKONDARI KISUMWA.
MWALIMU MKUU WA SHULE YA SEKONDARI KISUMWA ILIYOPO WILAYANI RORYA MKOANI MARA JOSHUA JOHN AKIONESHA BAADHI YA PAA ZILIVOEZULIWA NA KUTUPWA TAKRIBANI MITA 200 KUTOKA SHULENI HAPO.
BAADI YA MITI ILIYODONDOSHWA NA UPEPO MKALI.

Powered by Blogger.