Na: Frank Shija
MAKAMU
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan anatarajiwa
kuwa mgeni katika Mkutano Mkuu wa mwaka wa Chama cha Majaji Wanawake Tanzania
(TAWJA).
Hayo
yamebainishwa na Katibu wa Chama hicho Jaji C. W. Makuru kupitia taarifa yake
kwa vyombo vya habari aliyoitoa jana jijini Dar es Salaam.
Taarifa
hiyo imesema kuwa imesema kuwa Makamu wa
Rais anatarajiwa kuwa mgeni rasm katika Mkutano Mkuu wa nanw wa Chama cha
Majaji Wanawake Tanzania (TAWJA) utakaofanyika kesho (leo) jijini Dar es
Salaam.
Imeongeza
kuwa mkutano huo utafanyika katika ukumbi
wa PSPF Goldeni Jubilee Tower ghorofa ya nne na unatarajiwa kuanza majira ya
saa moja na nusu asubuhi kwa wageni waalikwa kuwasili na kujisajili.
Aidha
taarifa hiyo imeongeza kuwa Mkutano huo utatanguliwa na mafunzo ya uandishi wa
hukumu na elimu kuhusu mifuko ya jamii.
Kwa
mujibu wa taarifa hiyo mkutano huo unatarajiwa kuudhuriwa na wa wanachama ambao
ni Mahakimu na Majaji 200 kutoka pande zote za Tanzania.
Kauli
mbiu ya Mkutano huo ni “Ongoza njia
katika kufikia upatikanaji wa haki kwa wakati na kwa wote”.
|