AFISA UTUMISHI HALMASHAURI YA MJI WA TARIME, MUUGUZI HOSPITALI YA MJI WATUMBULIWA KWA UZEMBE.

MKURUGENZI  WA HALMASHAURI YA MJI WA TARIME ELIAS NTIRUHUNGWA AKIONGEA NA WATUMISHI WA SERIKALI IDARA TOFAUTI KUTOKA HALMSHUARI HIYO  KWENYE MKUTANO WA KAZI ULIOFANYIKA HII LEO KATIKA UKUMBI WA TARIME SEKONDARI.


WATUMISHI WA HALMASHAURI YA MJI WA TARIME MKOANI MARA WAKIMSIKILIZA MKURUGENZI KATIKA KIKIAO CHA KAZI HII LEO.


WATUMISHI WA HALMASHAURI YA MJI WA TARIME MKOANI MARA WAKIMSIKILIZA MKURUGENZI KATIKA KIKIAO CHA KAZI HII LEO.



 Mkurugenzi wa halmashauri ya mji wa Tarime mkoani mara, Elias Ntiruhungwa amemsimamisha kazi afisa utumishi wa halmashauri hiyo kwa kosa la uzembe wa kutekeleza majukumu anayopewa.

Akitoa taarifa hiyo kwenye kikao cha kazi na watumishi wa halmashauri ya mji wa Tarime alisema kuwa amefikia uwamuzi huo kutokana na afisa utumishi huyo Jeveryson Kaguna kushindwa kutimiza majukumu anayopewa na ofisi ya mkurugenzi kwa wakati.

Amesema kuwea kutokana na uzembe huo amesababisha watumishi kuidai halmashauri hiyo kiasi kikubwa cha fedha na kuwa tatizo hilo limewafanya wapoteze ari ya kufanya kazi.

“Unampa kazi na muda wa kuimaliza kazi hiyo, hatekelezi muda unaisha  na hatoi taarifa ya nini kimemfanya asikamilishe kazi hiyo, kama huwezi kazi andika barua ya kuomba kuachia ukuu wa kitendo ulicho nacho utaonekana wa maana kuliko kusubiria maamuzi kutoka juu,” alisema Ntiruhungwa.

Aidha amemsimamisha kazi Muuguzi wa hospitali ya mji wa Tarime Kegose Nega Jackson kwa kosa la kushindwa kutii agizo la mkubwa wake wa kazi la kusukuma kitanda cha mgonjwa.

“Huu ni utovu wa midhamu na hatuwezi kukubali tabia hii kuendelea, mwananchi wa kawaida hawezi kupeleka mgonjwa hospitalini na kufanya kazi ya wataalamu,´alisema Ntiruhungwa.

Akizungumza katika kikao hicho katibu tawala wa wilaya ya Tarime John Marwa amewaagiza watumishi wote wa serikali kutekeleza wajibu wao kwa kuzingatia sheria na taratibu za kazi ili kuepukana na matatizo yanayeoweza kuzuilika.

“Hakuna kiongozi anayemfukuza mtumishi kazi bali mtumishi anajifukuzisha kazi mwenyewe kwa kushindwa kutimiza wajibu,” alisema Marwa.

Wakizungumza katika kikao hicho kilichojumuisha watumishi wa Elimu, Afya, watumishi wote wa idara katika halmashauri ya mji wa Tarime, watumishi wameonyesha kufurahia hatua iliyochukuliwa na mkurugenzi huyo.

“Huu ni wakati wa kuchapa kazi hatua aliyoichukua mkurugenzi ni sahihi na inapaswa kuwa fundisho kwa wengine tuliobaki, ukitimiza wajibu wako hakuna mtu atakayekugusa,” alisema Samson Marwa.




AFISA ELIMU MSINGI YUSUPH MARWA AKIONGEA NA WATUMISHI WA HALMASHAURI WAKIWEMO WALIMU.
WA NNE KUTOKA KUSHO NI MKURUGENZI WA HALMASHAURI YA MJI WA TARIME ELIAS NTIRUHUNGWA WATAU KUTOKA KUSHOTO PIA NI KATIBU TAWALA WILAYA YA TARIME JOHN MARWA
KATIKATI KWA NYUMA NI MKUU WA IDARA YA UTAWALA NA UTUMISHI SHATI LA DRAFTI JEVERYSON KAGUNA BAADA KABLA YA KUTUMBULIWA HII LEO NA MKURUGENZI WA HALMASHAURI YA MJI WA TARIME ELIAS NTIRUHUNGWA WA KWANZA KULIA
MMOJA WA WALIMU AKIKABIDHIWA CHETI NA KATIBU TAWALA WA WILAYA JOHN MARWA KATI YA SHULE NANE ZA HALMASHAURI YA MJI ZILIZOFANYA VIZURI AMBAPO HALMASHAURI YA MJI WA TARIME IMEKUWA YA KWANZA MATOKEO YA DARASA LA SABA MWAKA JANAN KIMKOA KATIKA MKOA WA MARA.
PICHA YA PAMOJA WALIMU WA SHULE ZA MSINGI NANE ZILIZOFANYA VYEMA NA SHULE HIZO IKIWEMO SHULE MOJA YA BINAFSI AMBAYO NI ST JUDE NA NYINGINE ZA SERIKALI, NYAMISANGURA, RONSOTI, MTAHURU,NKENDE, TURWA,TARIME S/M NA KEMANGE.
KATIBU TAWALA WILAYA YA TARIME JOHN MARWA AKIONGEA NA WATUMISHI WA HALMASHAURI YA MJI WA TARIME  
Powered by Blogger.