Watu wawili wamefariki dunia wanne wajeruhiwa kutokana na
ajali baada ya gari walilokuwa wamepanda kuacha njia na kupinduka huku mtu mmoja aliyejulikana kwa jina la George Athuman Mwita 27 mkazi wa kijiji cha kerende wilayani Tarime
aliuawa kwa kupigwa na Mawe na wanachi wenye kujichukulia sheria mkononi baada
ya marehemu kumjeruhi mtu mmoja
aliyejulikana kwa jina la Marengo Mwita
32 mkazi wa kijiji cha kewanja kwa kumkata na panga mkono wa kulia kwa sababy
ambazo hazijajulikana.
Kamanda wa
polisi Mkoa wa kipolisi Tarime Rorya
Andrew Satta amedhibitisha kutokea kwa matukio hayo huku akisema kuwa tukio la
kwanza la gari aina ya Misitubishi Canter yenye namba za
usajiri T 937DFG mali ya Edward John
mnamo tarehe 6 06 2016 katika
barabara itokayo shirati –Tarime kitongoji cha Nyawita kijiji cha Lolwe Kata ya Kinyenche Tarafa ya
Nyancha Wilayani Rorya mkoani Mara gari hili likiwa limebeba abiria sita
likitokea shambani kubeba mazao lili acha njia na kupinduka na
kusababisha vifo vya wati wawili papo kwa papo na watu wanne kujeruhiwa.
Kamanda
amewataja walikufa kuwa ni Godfrey Sila mjaluo 30 mkazi wa nyamisambala,
Ponsian Vitus 40 muha mfanya bihasara na
mkzi wa Tarime na Majeruhi ni Esther Julius
27 mkurya na mfanya bihashara mkazi wa
Tarime Marwa Makuli mkurya35, Shimo Lameck 25 na Giribe John
Mfanyabihashara wote ni wakazi wa Tarime Mkoani Mara.
Majeruhi hao
wamelazwa katika Hospitali ya KMT Shirati kwa
matibabu na miili ya marehemu imeifadhiwa hospitalini hapo Dereva
ametoroka baada ya ajali hiyo na juhudi za kumutafuta zinzendelea na chanzo cha
ajali ni mwendo kasi.
Tukio linguine
kamanda amesema kuwa mnamo tarehe 06 06
2016 katika kitongoji cha nyamikoma kata
ya Matongo Tarafa ya Ingwe Wilayani Tarime Mkoani Mara Mtu mmoja aliyejulikana kwa jina la George
Athuman 27 mkurya na mkulima mkazi wa kijiji cha Kerende aliuawa kwa kupigwa
mawe sehemu mbalimbali za mwili wake na kumusababishia kifo na wanachi wenye
kujichukulia sheria mkononi.
Chanzo cha
tukio hilo ni Marehe baada ya kumjeruhi
mtu mmoja aliyejulikana kwa jina la
Marengo mwita 32 mkurya mkulima na mkazi wa kijiji cha Kewanja Wilayani Tarime Mkoani Mara kwa
kumkata na panga mkono wa kulia kwa
sababu ambazo hazikujulikana.
Kamanda wa
polisi Mkoa wa Kipolisi Tarime Rorya Andrew Satta ametoa wito kwa wanachi kuacha kujichukulia
sheria mkononi na badala yake wafikishe mtuhumiwa katika vyombo vya sheria huku akiwataka madereva wa vyombo vya
moto kufuata sheria za usalama barabarani ili kuepuka vifo vya mara kwa mara na
baadhi yao kubakia vilema wa kudumu.
|