Wafanya bihashara wajitokeza kumuchukulia Nyambari Fomu ya kuwania jimbo la Tarime Mara ya pili.

Katikati ni moja kati ya wafanyabihashara kutoka mji mdogo wa Sirari Mustapha Murimi kwa jina maarufa Masafa akikabidhiwa Fomu na  Katibu wa Chama cha Mapinduzi Wilayani Tarime Mkoani Marakwa niaba  ya Mbunge wa Jimbo la Tarime Nyambari Nyangwine ili aweze kutetea kiti chake cha Ubunge baada ya Jimbo kugawanywa na kuwa atawania jimbo la Tarime Vijijini..




   


Wafanya bihashara wajitokeza kumuchukulia Nyambari Fomu ya kuwania jimbo la Tarime Mara ya pili. 
                                Tarime.
Wilayani Tarime Mkoani Mara wafanyabihashara wa mji mdogo wa Sirari wamejitokeza kumuchukulia fomu ya kuwania ubunge awamu ya pili aliyekuwa Mbunge wa jimbo la Tarime Nyambari Nyangwine kwa kile ambacho wamedai kuwa katika uongozi wake wa miaka mitano ameweza kukomesha vita vya koo kwa koo, kuleta Huduma ya Umeme pamoja na Baranarakupitika kila mahari suala ambalo limezidi kuwapa imani wananchi hao.

Wafanya biashara hao wamedai kuwa kabla ya Mbunge huyo kuongoza jimbo la Tarime kulikuwepo na vita vya koo na na koo wezi wa mifugo lakini kwa sasa suala hilo limeisha nawananchi kuishi kwa amani suala amblo wanajinunia kwake ambapo wameamua kumurudishia fadhila kwa kumuchukulia fomu ili aweze kuwania jilmbo hilo kwa kutetea kiti chake na hapa wafanya biashara wanaeleza kile kilichowasukuma kumuchukulia fomu mbunge huyo.

Wakichukua fomu katika ofisio ya chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ili mbunge huyo aweze kuwania jimbo la Tarime vijijini huku akitetea kiti chake baada ya majimbo hayo kugawanywa mara mbili kuwa na jimbo la Tarime Vijijini naMmoja wa wafanya bihashara hao Mustapha Murimi Marufu kwa jina la Masafa  alidai kuwa wameamua kumuchukulia fomu na kujaza ili waweze kurudisha baada ya kuona  utendaji wake mzuri  katika kipindi chake ambacho alipewa takribani miaka mitano.

Kwa Upnde wake Marwa Mukare alisema kuwa wakati Bunge huyo kipindi anachukua Ubunge kulikuwepo na Vita vya koo na koo lakini baada ya kuchukua Ubunge suala hilo limeisha pia ameweza kuchangia kwa kiasi kikubwa kugawanywa kwa majimbo kwa lengo la kupanua wigo na kuwaletea wananchi maendeleo kwa ujumla.

“Kabla hajachkua Ubunge Nyambari kulikuwa na vita baina ya Wairege na  na Wanyabasi wanchari na Wakira lakini hayo yote yameisha na sasa tunaishi kwa amani hiyo tumeamua kumurudisha hawamu ya pili ili kumalizia baadhi ya vipolo vyake ambavyo vimebaki na kuleta maendeleo”alisema Marwa.

Kwa sasa wilayani Tarime Mkoani Mara baada ya Tume ya Uchaguzi kugawanya majimbo nakuwa na jimbo la Tarime Mjini yenye kata nane na Tarime Vijijini yenye kata 26  hivyo itabidi Wilaya hiyo kuwa na wawakilishi wawili kwa lengo lakuwaletea wananchi maendeleo.


Powered by Blogger.