UWT MUSOMA WAASWA KUSHIKAMANA KUSHINDA UCHAGUZI MKUU.


UWT  MUSOMA  WAASWA KUSHIKAMANA  KUSHINDA UCHAGUZI MKUU.
                                              Musoma
Umoja  wa  wanawake  wa Chama cha Mapinduzi  UWT wilaya ya Musoma  mkoa wa Mara, umeaswa kushikamana na  kuunganisha nguvu pamoja  hatua ambayo imetajwa  itakikifanya chama hicho  kupata ushindi katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwezi oktober mwaka huu.

Kauli hiyo imetolewa hapo jana na  msimamizi wa uchaguzi wa UWT wilaya ya Musoma Mjini  Amos Sagara  wakati akihitimisha zoezi la uchaguzi  wa Madiwani wa viti maalum  ndani ya umoja huo,  uliofanyika katika ukumbi wa chama cha mapinduzi CCM uliopo mjini Musoma mkoani Mara, ambapo jumla ya madiwani 6 wa viti maalum walichaguliwa watakao ungana na madiwani wa  kata ambao watachaguliwa katika uchaguzi mkuu.

Waliochaguliwa katika uchaguzi huo ni Neima Samson,Zainab Msiba,Amina Shabani,Meleciana Masungura,Rebeka Mkama, pamoja na Rose Magoti  ambapo wajumbe walioshiriki katika uchaguzi huo jumla yao walikuwa 300 kutoka katika kata kumi na sita za manispaa ya Musoma, ambapo mara baada ya kuchaguliwa  waliombwa kuwa chachu ya hamasa kwa wanawake wengine kukipigania chama hicho ili wakati wa uchaguzi kiweze kurejesha  jimbo hilo pamoja na manispaa ambayo ilikuwa ikiongozwa na chama cha Chadema.

Sagara aliwaomba wanawake wa UWT  wa wilaya hiyo, kuepuka makundi ambayo yamekuwa yakileta mpusuko  hususani nyakati za uchaguzi, na badala yake akawataka kushirikiana bega kwa bega  ilikuhakikisha  wanafanya  vizuri katika uchaguzi mkuu  ili kupata viongozi watakao  tatua  changamoto zinazo wakabili wananchi wa Musoma, ambazo hazikuweza kutatuliwa  na  serikali ya Chadema ililiyomaliza muda wake ambapo  changamoto katika sekta ya Elimu, Afya Miundombinu zikishindwa kupatiwa ufumbuzi yakinifu.

Aliongeza kuwa  ili chama hicho kiweze kushinda uchaguzi huo, ni lazima walioshindwa katika uchaguzi huo wa UWT wakubaliane na matokeo na kuwaunga mkono waliochaguliwa badala ya kutengana na  kulumbana  kwani  kwa kufanya hivyo watazidi kutoa mwanya wa kushindwa  na  hivyo kushindwa kufikia malengo ya kuwapata viongozi watakaotokana na CCM  ambao watatoa majibu ya kero za wananchi.

‘’Niwaombe sana  wagombea ambao mmeshinda katika uchaguzi huu, shirikianeni kwa pamoja na wenzenu ambao kura hazikutosha kukiimarisha chama  iliwakati wa uchaguzi muibuke washindi kwani sri kubwa ya kushinda ni kushikamana na kuweka pembeni  tofauti zenu  walioshindwa  nawaombeni sana nanyi  mshirikiane na walioshinda  kwani ushindi huu nio wa CCM siyo mtu binafsi’’alisema Sagara.

Awali   Kamese Magoti ambae  ni Mjumbe wa halmashauri kuu ya CCM mkoa wa Mara akitoa hotuba yake kwa niaba ya Mgeni rasmi Vedastus  Mathayo  ambae ni  MNEC  wilaya ya Musoma mjini,  aliwataka wanawake wa  umoja huo  kuwa makini katika chaguzi zinazofanyika ndani ya chama hicho ilikuwapata viongozi bora watakaopigania maslahi ya wananchi  na kusukuma mbele gurudumu la maendeleo kwa ufanisi mzuri sanjari na  utawala bora.

Aidha Kamese aliongeza kuwa  kwa wale watakaoshindwa katika chaguzi zinazofanyika ndani ya Chama wajifunze kuwa na uvumilivu wa kisiasa badala ya kuhama chama pindi wanaposhindwa  kwani kwa kufanya hivyo ni kuonesha ukomavu wa Demokrasia  ndani ya CCM tofauti na vyama vingine vya upinzania  hapa nchini.

Powered by Blogger.