Mwenyekiti wa baraza la vijana Chadema asema yeye ni Tumaini jipya kwa wanatarime.

Picha ya mwenyekiti wa Baraza la vijana BAVICHA  Chadema Wilayani Tarime Mosses Yomani akiongea na Mmiliki wa Blog hii kuhusiana na mustakabali wa kuwania jimbo la Tarime Mkoani Mara.

                                                Tarime.
Mwenyekiti wa baraza la vijana Chadema  asema yeye ni Tumaini jipya kwa wanatarime.

 Mwenyekiti wa Baraza la vijana Chadema   Wilayni Tarime Mkoani Mara   (BAVICHA) Moses Yomami ambaye pia ni mwanasheria wa Chama cha Demokrasia na maendeleo chadema Kanda ya Serengeti ambayo inajumuisha Mkoa wa Mara, Shinyanga na Simiyu amesema kuwa ameamua kutia nia ya kuwania jimbo la Tarime baada ya kuona rasilimali zilizopo katika mkoa wa Mara kutonufaisha wananchi baada ya viongozi ambao wamekuwa wakichaguliwa kutotumia vizuri vipaumbele vilivyopo.
Katika harakati za kutangaza nia  kwa lengo la kuwania jimbo la Tarime Mkoani Mara Bw :Moses misiwa yomami ni moja kati ya watiania hao huku akibainisha vipaumbele vyake na suala ambalo limemusukuma kuwania kiti hichi cha ubunge.
Moses alisema kuwa  yeye ni kijana ambaye ni tumaini jipya katika jimbo la Tarime hivyo wananchi hawana budi kufanya maamuzi yaliyosahii katika kumuchagua pale atakapopendekezwa na chama chake ili kuweza kupeperusha bendela ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA kwa lengo la kusukuma gurudumu la maendeleo kwa kushirikisha wananchi wotena rasilimali zao.

Akiongea na gazeti hili Mtia nia huyo alitoa historia yake kuwa Bw moses  aliyezaliwa kijijini nyamwaga mwaka 1987 wilayani Tarime  ana shahada ya sheria kutoka chuo kikuu cha mtakatifu agustine jijini mwanza na kwa sasa ni miongoni mwa wanasheria wa chama hicho katika kanda ya Serengeti.
Kiongozi huyo aliongeza kuwa kutokana  na wilaya hiyo kuwa na ardhi nzuri na mvua za mara kwa mara kipindi cha masika ikiwa ni pamoja na kuwa na madini mengi lakini bado rasilimali hizo hazimnufaishi mwanachi wa kawaida kwa kiasi cha kuridhisha ameamua kuwania kiti hicho ili akiweza kupata fursa aweze kuzitetea kwa lengo la kuwaletea wananchi maendeleo.

 “Changamoto za elimu,upungufu wa walimu,vifaa vya kufundishia  mashuleni,usimamizi mbovu wa mapato ya halmashauri ulipaji mbovu wa kodi kwenye makapuni ya uwekezaji tuliyonayo,sekta ya afya ni aibu madawa hamna,uhaba wa manesi,madaktari na majengo  mabovu,sekta ya kilimo na mifugo hatuna ofisi za watalamu wa kilimo na mifugo ingawaje tunasikia kuna vyuo vikuu vya kilimo kama sua lakini bado wananchi wanakufa na umskini” alisema Mwenyekiti.
Anabainisha kwamba wilaya ya Tarime inalima mazao ya chakula na biashara ambayo yana soko katika upande mwingine wa Afrika mashariki hasa nchini Kenya lakini  ni vigumu kwa wananchi kusafirisha mazao hayo kutokana na vizuizi vilivyowekwa.
Hivyo alisema  kuwa atatumia jukwaa la majadiliano kwa lengo la kuona mwananchi  ananufaika na rasilimali inayomzunguka ikiwa ni pamoja ya kupigania utetezi katika kuwepo kwa mikataba yenye tija kwa mwananchi kupitia  makampuni ya uchimbaji madini.
Moses yomami anasema akiwa kiongozi wa wanafunzi wa vyuo vikuu kutoka vijiji vinavyozunguka mgodi wa acacia uliopo Nyamongo Wilayanio Tarime Mkoani Mara waliokuwa wakisomeshwa na kampuni hiyo,amebaini kumekuwepo mabadiliko ya majina ya kampuni hiyo ya madini huku wakurugenzi wake wakiwa ni walewale kitendo kinachoashiria kuwepo kwa udanganyifu katika ulipaji wa mapato serikalini anabainisha pia kuwa akiwa bungeni atashawishi bunge kwa hoja binafsi kubadili mfumo wa sheria za kodi na misamaha ya kodi kampuni za madini  zinalipa asilimia 0 kwenye bidhaa zinazotoka nje ya nchi lakini za uchimbaji wakati wa utafiti mpaka mwisho na mpaka mwishoni mwa mwaka wa kwanza wa uzalishaji na baada ya hapo wanalipa 5% kampuni hizi pia  zinalipa asilimia 0% kama kodi ya mafuta wanayoagiza nje.
Aliongeza kuwa pamoja na mgodi huo wa acacia kusomeshwa vijana kwa elimu ya chuo kikuu,atanzisha mjadala na kampuni hiyo iweze kusomesha wanafunzi wote wa sekondari kama ambavyo tumejadili wameanza kijijini nyamwaga kulipia wanafunzi hao kwani kilakitu kinawezekana ukiweka mkakati safi.
………Mwisho….

                  
Powered by Blogger.