Mgombea Udiwani kata ya Nyanungu atoa vipaumbele kwa vijana.

Katibu wa Chama cha mapinduzi kata ya Nyanungu akikabidhi fomu kwa mgombea wa udiwani kata ya Nyanungu Marwa Daud Ngicho hap jana


                                         Tarime.

Mgombea Udiwani kata ya Nyanungu atoa vipaumbele kwwa vijana.

Mmilikiwa Mgodi wa wachimbaji wadogo Mosege uliopo nyamongo wilayani Tarime Mkoani Mara Marwa Daudi Ngincho ambaye kwa sasa ameingia katika ulingo wa siasa kwa lengo la kuwaletea wananchi wake maendeleo baada ya kuona uongozi uliopo ndani ya kata  kutotenda haki kwa wananchi wake ikiwa ni pamoja na ukosefu wa huduma ya Afya, Maji na Elimu,


Akichukua Fomu ya kuwania Udiwani kata ya Nyangungu Ngicho alisema kuwa ameamua kuwania kiti hicho kwa lengo la kupata nafasi hiyo ili kuendelea kusaidia vijana Akina Mama na wzee ili kila mtu aweze kuwa na maisha mazuri na siyo tegemezi kwa kila kitu.


Alisema kuwa kabla ya kuwa kiongozi kupitia mgodi wake wa wachimbaji wadogo uliopo Mosege ameweza kutoa ajilia kwa vija zaidi ya 420 ambao pia walikuwa wakijiusisha na suala zima la uwindaji haramu katika Hifadhi ya Mbuga ya wanya Serengeti.


Aidha daud aliongeza kuwa ameweza kufungua vikindi nane vya akina mama na kuviwezesha pesa ili viweze kujiendesha lengo kubwa ni kubadili maisha ya wakazi wa kata ya Nyanungu.


“Uongozi ambao tulichagua katika kipind kinachomalizika ulikuwa ni  CHADEMA alakini hawakuweza kuwatetea wananchi sasa lazima wananchi wafanye mahamuzi yaliyo sahihi  ili kuleta kiongozi aliyebora” alisema Ngicho. 


Kwa upande wake Mwenyekiti wa kata ya Nyanungu Damian Munge aliongeza kuwaKatika kuleta na kudumisha amani hapa Nchini  kwenye mchakato ulipo mbeleni wa uchaguzi wa Madiwani Wabunge na  amewaomba viongozi mbalimbli wakiwemo viongozi wa kiserikali kusimamia haki katika uchaguzi huo ikiwa ni pamoja na kuondokana na siasa zenye maji taka kwa lengo la kuwaletea wananchi maendeleo.


Kauli hiyi imetolewa na mwenyekiti huo katika ofisi ya chama kata kipindi Kipindi  cha mgombea huo anaye wania kiti cha udiwani  kupitia CCM  kata ya Nyanungwa Marwa Daud Ngicho alipokuwa  akichukua fomu ofisini hapo.


Powered by Blogger.