MATIKO MWANAMKE ANAYETHUBUTU.

MATIKO MWANAMKE ANAYETHUBUTU.
                                  Tarime
HATUA ambayo Taifa letu limefikia kuhakikisha sharia inayoyatambua makundi maalu,wanawake,walemavu na Vijana ili kujitokeza kugombea nafasi mbalimbali za uongozi inatekelezeka ni nzuri.

Kufuatia sheria hiyo kupewa msukomo na serikali na jamii kupatiwa  elimu na mashirika mbalimbali yakiwemo yasiyokuwa yaserikali kuwa wanawake,walemavu na Vijana wanayo haki sawa kwa jamii na wanawajibu wa kuwa viongozi baadhi ya watu kutoka makundi hayo wamejitokeza kuchukua fomu katika vyama vyao ili kugombea nafasi mbalimbali za uongozi. 

Hali hiyo imedhihirika kuwa jamii ya Kiafrika kwa sasa hatua iliyofikia ni nzuri kwa kutoa nafasi ya kuruhusu makundi hayo bila kikwazo kuchukua fomu na kurusha karata ya kinyang'anyiro cha kuchaguliwa na kuwa kiongozi.  

Katika Wilaya Tarime na vitongoji vyake sharia hii imewapa nafasi baadhi ya wanawake,vijana na walemavu kujitokeza kugombea baada ya vyama wanavyotoka kuwapa ridhaa ya kuchukua fomu.
Aidha katika Wilaya Tarime mwanamke pekee ambaye ameonye  ujasiri wa kujaza fomu ili kingia katika mchakato wa kura za maoni hatimaye kugombea Uongozi ngazi ya Ubunge ni Esther Matiko ambaye ni Mbunge viti maalumu Mara kupitia tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA.

Matiko amesema atakuwa mwanamke wa kwanza kutoka upinzani ambaye atachukua fomu ykuomba ridhaa kutoka ndani ya chama chake ili kumpitisha na kugombea nafasi ya Ubunge uchuana na upande wa pili CCM kwa yeyote watakaye mleta.

Aidha wengine ambao wanatajwa kuwa atchukua fomu na kurusha karata katika nafasi ya kugombea Ubunge katika jimbo mojawapo baada ya kugawanywa na kuwa majimbo ya uchaguzi  ni Chirstopha Kangoye wa Chama cha mapinduzi.

Wengine wanaotajwa katika kujarbu karata katika nafasi hiyo ni John Heche kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA,Peter Busene(CHADEMA)Mbunge wa sasa Nyambari Nyangwine wa CCM Michael Kembaki wa CCM Johanes Manko CHADEMA na Charles Mwera wa CUF.
Licha ya kuwa majimbo yamegawanywa kutoka jimbno moja la uchaguzi na kuwa majimbo mawili  Mbunge Matiko ameonyesha kuwa na umahiri mkubwa kisiasa huku akifuatiwa na Kangoye kwa sababu ya michango anayoendelea kuitoa ndani ya jamii ya Tarime bila itikadi hali ambayo imemjenga  na kumpa umaarufu wa kisiasa.

Kwa hatua nyingine mtia nia wa kugombea Ubunge Chirstopha Kangoye wa Chama cha mapinduzi CCM amejijenga kisiasa huku wananchi  wa Tarime wakidai kuwa wanahitaji Mtu kama huyo ambaye anatoa misaada kwa wananchi na kuwapunguzia ukali wa garama za michango mbalimbali inayowasibu.

Kangoye amewahi kutoa misaada ya vitanda kwa wagonjwa katika hospitali ya Tarime mkoani Mara na kupunguza uhaba uliokuwepo na wagonjwa kupata mahali pazuri pa kulala wakati wakiwa hospitalini hapo kutibiwa.
Kwa hali hiyo mafahari hao wawili Kangoye wa CCM na Matiko wa CHADEMA jamii imetokea kuwaamini huku wakisubiri vyama vyao kuwachagua na kuwapitisha ili kuingia katika mchakato kinyang'anyiro cha kupambana na wengine  ambayo watakuwa wameomba kuygombea nafasi hiyo.

Esther Matiko amesema kuwa kama chama chake kikimpitisha atahakikisha anaungana na wananchi wa Tarime kuwaletea maendeleo bila kujali itikadi ya vyama.

Matiko ameonyesha mwanga wa maendeleo katika jamii na kuwatia nia wanawake kujitokeza kwa wingi kugombea nafasi mbalimbali za uongozi na kuondokana na dhana potofu kuwa mwanamke hawezi. 

Kwa  upande wake Rebeka Mjema kutoka shirika lisilo la kiserikali TGNP wakati wa semina moja ilyofanyika mwaka jana mjini Morogoro  alisema kuwa jamii ikielimishwa na kuondoka na fikira mgando zinazo tokana na mifumo mibovu ya kiutawala pamoja na mila potofu watafikia lengo asimia 50 kwa 50 katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwaka huu Okotbar 2015. 

Aidha Mjema aliongeza kuwa waandishi wahabari wanayo nafasi ya kutumia kalamu zao kuelimisha jamii kuondokana na thana potofu ya kiubaguzi inayofanywa na jamii kukuza makundi hayo kujitokeza kushiriki kugombea nafasi mbalimbali za uongozi. 

Mjema alisema kuwa  tamko la umoja wa mataifa la haki za binadamu UDHR(1948) na ICCPR(1978)Ushiriki kama haki umeainishwa kuwa ni kushiriki katika maswala yote ya jamii moja kwa moja au kwa kupitia wawakilishi kuchagua na kuchaguliwa katika chaguzi.

Jambo jingine sheria ya vyama vya Siasa ya mwaka 1992 kifungu cha 8(10(c) inasisitiza uwepo wawanachama wa jinsia zote na uwakilishi wa makundi yote katika chama.    
 ....................................................................mwisho,,,,,,,,,,,,,,


Powered by Blogger.