WAANDAMANA IDARA YA MAJI KUDAI MALIPO WATAKA MUHASIBU AFUKUZWE KAZI.

WAANDAMANA  IDARA YA MAJI KUDAI MALIPO WATAKA MUHASIBU AFUKUZWE KAZI.


WAFANYAKAZI  8 wa Idara ya Maji na Usafi wa Mazingira Wilayani Tarime mkoani Mara ambao ni vibarua wameandamana hadi ofisi za Maji kudai mishahara yao ya mwezi uliopita jambo ambalo wamesema limesababisha watoto wao wasiende shule kwa kukosa ada.
 
Wakizungumza na gazeti ili nje ya Ofisi za idara ya Maji walisema kuwa Uongozi wa  uliopo sasa wa Idara  chini ya Muhasibu wake  Haruni Kituri  Amekuwa na mazoea ya kuwacheleweshewa malipo huku akidaiwa kuwapunja mishahara yao tofauti na uongozi uliopita wa Marehemu aliyekuwa Meneja wa Maji Sebastian Swima.
 
“Tunatakiwa kulipwa mishahara au malipo yetu kila ifikapo 28 lakini mwezi unapitiliza hadi sasa hatujalipwa fedha,Uongozi wa Marehemu Meneja Swima tulilipwa kwa wakati na mshahara ulikuwa  laki 273,000 lakini sasa wamepunguza hadi laki 250,000”Alisema Kichere Chomete (40) Dereva wa Gari la Idara ya Maji.
 
Joseph Iroma (43) Mkazi wa Mtaa wa Kenyamanyori amabye ni milinzi  wa  mashine ya maji Lambo la maji la Kenyamanyori kwa miaka 4 alisema kuwa wanazungushwa malipo kwakuwa hawana mikataba ya kazi na amekuwa akilinda mashine bila kuwepo kwa umeme na kumpa wakati mgumu kazini.
 
“Ungozi Uliopo unasema sisi hatujasoma! Nawakati watu wamefanya kazi zaidi ya miaka 10 na bado ni vibarua kwahiyo wanataka watu wenye digree ndio waje wachimbe mitaro ya kuweka mabomba! Huu ni unyanyasaji tumeshindwa hadi kupeleka watoto shule” anasema Iroma.
 
Kaimu Meneja wa Idara yamaji safi n usafi wa mazingira ambaye pia ni Muhandisi wa Maji Halmashuri ya mji Tarime Dickson Kamazina alikiri kuwa ni kweli Vibarua wamekuwa wakicheleweshewa malipo Tangu mwezi Novemba,2014.
 
Kamazina Alisema kuwa sababu ya kucheleweshwa kwa malipo inatokana na  makusanyo madogo ya maji na kuna wateja wa maji 1,500 ambao hata hivyo wengi wao wana madeni ya maji na hawalipi fedha nakwamba  hakuna ruzuku kwenye idara hiyo.
 
“Mimi ni Mgeni nimeingia Novemba nikakuta vibarua walikuwa hawajalipwa fedha za Novemba nikashughulika ndani ya mwezi mmoja kulipa malipo ya miezi miwili, na makusanyo ni madogo tunakusanya milioni 6 na tunawatumishi 18 malipo ni zaidi ya milioni 5 “alisema Kamazina.
 
Anaongeza”Fedha hizo hizo bado tulipe ada, na matumizi ya umeme na mengineyo Hatuna ruzuku unakuta fedha haitoshi inabidi ukusanye ikikamilika ndiyo ulipe vibarua ila leo hii watawekewa fedha zao kwenye akaunti.
 
Akizungumiza Mikataba Kamazina alisema kuwa amekuta vibarua hawana mikataba na sasa ana anadaa mikataba ya vibarua  nakwamba vibarua si waajiriwa na malipo yao ni sh.8,000 kwa siku ambayo  kuzikusanya na kulipwa baada ya mwezi, na kila mtu analipwa kulingana na siku alizofanya kazi  nakwamba malipo yanatofautiana kulingana na miezi na siku walizofanya kazi.
 
Hata hivyo Mgumo Adrea alisema kuwa anasikitika licha ya kufanya kazi kwenye idara hiyo ambayo ni ya Serikali bado analipwa kama kibarua, nakwamba malipo ya 8,000 yalishapanda ambapo kwa uongozi uliopita kila mtu alilipwa sh. Laki 273  elfu kwa kila mwezi.
 
…………………………………………….MWISHO
Powered by Blogger.