Wawili wafariki dunia katika ajali za Barabarani
Wawili
wafariki dunia katika ajali za Barabarani
WATU wawili
akiwemo Mwanafunzi wa Darasa la tano Shule ya msingi Rwang’enyi Wilayani Rorya
Mkoani Mara wamefariki Dunia kwa nyakati tofauti wakihusishwa Ajali za
Barabara.
Akizungumzia
matukio hayo Kamanda mkoa wa kipolisi Tarime/Rorya ACP Lazaro Mambosasa alisema
kuwa tukio la kwanza Mwanafunzi wa Darasa la tano shule ya msingi Rwang’enyi
Benjamin Ismail 13 amefariki dunia Desemba10,2014 akiwa anapatiwa matibabu
katika hospitali ya KMT iliyopo Shirati baada ya kugongwa na mwendasha pikipiki
ambaye hakujulikana na kjumsababishia majeraha sehemu za kichwani.
Kamanda huyo
aliongeza kuwa Marehemu alikugongwa wakati akiwa anaenda shuleni kusoma wakati
akiwa amepanda baisikeli anaendesha majira ya saa mbili asubihi.
Aidha
Mambosasa aliongeza kuwa marehemu aligongwa na mwendesha pikipiki ambaye jina
lake halikujikana na pia namba za usajili wa pikipiki hazikujulikana kwa
urahisi kwa kuwa baada kuwa amegonga alikimbia na jeshi la pilisi linafanya
jitihada za kumsaka na kumkamata ili kumfikisha kunako husika.
Tukio
jingine Mambosasa alisema kuwa pikipiki yenye namba za usajili MC 459 KBT aina
ya SUNLG iliyokuwa ikiendeshwa na Daud Kinyunyi 20 mkazi wa kijiji cha Kabwana
alimgonga mtembea kwa miguu Juma Peter 5 mkazi wa Raranya na kumsababishia kifo
pao hapo.
Katika tukio
hilo kamanda amesema kuwa Mtuhumiwa amekamatwa na atafikishwa mahakamani ili
kukabiliana na sheria punde upelelezi utakapo kamilika.
‘’Natoa wito
kwa madereva wanaoendesha vyombo vya moto kufuata sheria na kanuni za usalama
barabarani ili kuepusha vifo vya mara kwa mara na majereha na hata uharibifu wa
vyombo vyao’’alisema Mambosasa.