Zaidi ya vijana 250 wamepata ajila kupitia uchimbaji mdogo.

Wachimbaji wadogo katika mgodi wa Musega kijiji cha Genkuru kata ya Nyarukoba wilayani Tarime 
Mkoani Mara  wakiponda mawe kwa ajili ya kuuzia wateja na badae kupembua na kupata  dhahab



Zaidi ya vijana 250 wamepata ajila kupitia uchimbaji mdogo.
Zaidi ya vijana 250 wakiwemo wakina mama, na wazee wamepata ajila katika mgodi wa wachimbaji wadogo wa Musega uliopo katika kijiji cha Genkuru kata Nyarukoba Wilayani Tarime Mkoani Mara suala ambalo limewasaidia kukidhi mahitaji yao huku baadhi ya vijana wakiondokana na uvamizi wa migodi pamoja na uwindaji haramu ambao walikuwa wakifanya hapo awali kabla ya kupata ajila hizokatika vijiji ambavyo ni jirani na hifadhi ya Mbuga ya wanyama
Akiongea na Gazeti hili mmoja wa wamiliki wa Mgodi huo Ngicho Daud alisema kuwa ameweza kuajili vijana zaidi ya 250 wakiwemo wazee na akina mama.
“Kwa upande wa vijana tumewaajili kwa lengo la kupunguza uvamizi wa migodi pamoja na uwindaji haramu kwa sababu hapa wanafanya kazi masaa yote nakujipatia kipato kikubwa”alisema Ngicho.

Aliongeza kuwa  mgodi huo ulianzishwa na watu watatu lakini mpaka sasa watu wengi wameweza kujipatia ajila kupitia mgodi huo japo anakumbwa na changamoto kama vile ukosefu wa vifaa vya kisasa, ,Maeneo ya kutosha , Mtaji mkubwa kwa ajili ya kupanua Miradi ya uchimbaji huo.
 Sibute Masero ni mmoja wa vija ambao wamepata ajilia kupitia mgodi huo wa wachimbaji wadogo alisema kuwa ameamua kuacha suala la uwindaji haramu na kujiingiza katika uchimbaji mdogo kwa lengo la kupata kipato cha harari.
“Katika uwindaji haramu niliweza kufungwa kilia gereza lakini nilifanikiwa kutoka hivyo  inabidi niendelee na kazi yangu ya uchimbaji mdogo ili kupata kipato changu” alisema Sibute.
Kwa upande wake Pusinya Kichugu mkazi wa Kijiji cha Genkuru alisema kuwa kutokana na kununua mawe hayo ameweza kusomesha watoto wawili sekondari na kukidhi mahitaji yake yote ya Nyumbani.
                        
Wakina mama tuliowengi tunategemea Machimbo haya madogo kikubwa tunaomba serikali iltuletee  vifaa vya kisasa ili tuweze kuboresha uchimbaji wetu alisema Pusinya
                               ….MWISHO…
 
Powered by Blogger.