wauana wakigombania Ardhi. Ndugu
MKAZI wa kitongoji cha Nyamirungu Kijiji cha Magoma
kata ya Binagi Wilayani Tarime Mkoani Mara ameuawa kwa kukatwa mapanga na ndgu
wa Damu wakigombania Mipaka ya Ardhi
Akisimlia
tukio hilo kwa waandishi wa habari Ofisini kwake Kamishina msaidizi wa Jeshi la
polisi wa Mkoa wa kipolisi Tarime/Rorya Lazaro Mambosasa alisema kuwa tukio
hilo lilitokea November,14 mwaka huu majira ya saa 2.00 asubuhi.
Aidha
Mambosasa alimtaja marehemu kuwa ni Samweli Mgaya Waitte 44 ambaye aliuawa na
Mkubwa wake Chacha Mwita Waitte 56 wakati wakigombania mipaka ya Ardhi na kuwa wote
ni wakazi wa Kijiji cha Magoma.
Mambosasa
aliongeza kusema kuwa baada ya ugomvi huo kutokea Mtuhumiwa alimshambulia kwa
mapanga marehemu ambapo alishambuliwa kwa kukatwa sehemu mbalimbali za mwili
wake ikiwemo kichwani na tumboni na kusababisha kifo chake papo hapo.
;;Marehemu alimkata mapanga mtuhumiwa na kumjeruhi sehemiu mbalimbali za mwili wake
hali ambayo ilisababisha kwenda kulazwa katika hospitali ya halmashauri ya Mji
wa Tarime akiwa chini ya uangalizi wa polisi ili akipona akahojiwe;;alisema
Mambosasa.
Kamanda huyo
ameitaka jamii kuacha tabia ya kujichukulia sheria mkononi badala yake wapeleke
matatizo katika vyombo vya sheria hususani katika mabaraza yanayo husika na
Ardhi ya vijiji ili kuweza kutatua migogoro inayowakumba.
,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,mwisho,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,