Akina Mamajitokezeni kugombea Uongozi.

Akina mama wametakiwa Kujitokeza katika kugombea uongozi kupitia  nyadhifa mbalimbali ili kuweza kutetea haki zao za ,msingi ikiwa ni pamoja na kutimiza haki ndoto zao za uongozi.

Kauli hiyo imetolewa na aliyekuwa mbunge wa Jimbo la Tarime na Halmashauri ya willaya ya Tarime ambaye kwa  sasa ni Diwani wa kata ya Itiryo Charles Mwera Nyanguru kipindi akiongea na gazeti hili.

Charles alisema kuwa akina mama hawana budi kuchukua fomu za kugombea katika chaguzi za serikali za mitaa kwani wanawake wamekuwa wakipoteza fursa ambazo ziko wazi kwa kuogopa kugoimbea.

“Wakina mama wakigombea watatumia fursa hizo kuzidi kutetea haki zao za msingi na si kutegemea wanaume kwa kila kitu” alisema Nyanguru.
Hata hivyo Mwera aliwataka vijana kujitokeza kwa wingi kujiandikisha katika Daftri la kudunmu la wapiga kura.

“Kujiandikisha katika daftari ndo nguzo kubwa ya kukufanya upige kura na kupata kiongozi bora hivo basi vijana wajitokeze katika kujiandikisha kuanzia 23 novemba mpaka 29 novemba  mwaka huu alisema” Mwera.

Aaidha aliongeza kuwa vijana ndio tegemeo la taifa hivyo waondokane na ushabiki wa vyama na kufanya maamuzi yaliyoya kweli katika kuchagua viongizi waliobora ili kuletea Taifa maendeleo.

“Naweza kutoa msisitizo kuwa na vijana waweze kujitokeza kuchukua fomu za kugombea si kuwaachia wazee tu” alisema .
                                 ….MWISHO…

Powered by Blogger.