Ligi ya Mbunge wa viti maalumu kutimua vumbi Novemba 23.




Ligi ya Mbunge wa viti maalumu kutimua vumbi Novemba 23.

Kupitia rigi ya Ester Matiko Tarime  Football Rising  Stars Cup 2014- 2015ambaye ni mbunge wa viti maalumu  tiketi ya chama cha Demokrasisia na maendeleo Chadema  itaanza kutimua vumbi  kuanzia 23 novemba  katika viwanja tofauti kwa kukutanisha timu mbalimbali za kata 32 zilizomo ndani ya Mji wa Tarime na wilaya  Tarime Mkoani Mara kwa lenngo la kusaka vipaji kutoka maeneo ya Vijijini.

Awali ya hapo mdhamini wa mashindano hayo ambaye ni mbunge vwa viti maalumu Jimbo la Tarime Ester Matiko  ameweza kutoa mpira mmommoja kwa kila timu kupitia timu32 kwa ajili ya mazoezi kabla ya kuanza kwa  michuano hiyo.Ester Matiko amesema kuwa ameamau kuanziusha ligi hiyo ili kuweza kukutanisha vijana huku wakiibua vipaji vilivyojificha na kutengeneza timu moja atakayoiendeleza mpaka inashiriki michuano ngazi ya mkoa.

“Lengo langu ni kuibua vipaji na kuweza kupata timu moja ili niweze kuiendeleza ili iweze kucheza katika ngfazi ya mkoa” alisema Matiko.

 Martini Kebacho ni Mratibu wa michuano hiyo wakati akikzungumzia michuano hiyo alisema kuwa ratiba tayari imetolewa kwa timu zote32 ambazo zitashiriki awamu ya kwanza ili kupata timu16 na kucheza hawamu ya tatu ili kupata timyu8 ambazo zitaanza ligi ili kupata mshindi wa kwanza mpaka wa tatu.

Mdhamini swa mashindano hayo alisema kuwa mshindi wa kwanza atajinyakulia kitita cha shilingi million moja na kombe  Mshindi wa pili Laki saba na mipira miwili, huku Mshindi wa tatu akijinyakulia na mpira mmoja na zawadi mbalimbali kwa wachezaji bora, wafungaji bora na walinda miilango bora.

Hata hivyo matiko amewataka wananchi kutoingiza siasa kwa kutumia itikadi za vyama bali washiriki mashi ndano hayo ni kwa watu wote ili kuweza  kusaka vipaji kupitia timu za vijijini.
                                           ….Mwisho…
Powered by Blogger.