Kiribo limited watoa msaada wa Mllioni 2.5.



Kiribo limited watoa msaada wa Mllioni

Katika kuunga juhudi za serikali ili kuboresha sekta ya Elimu kupitia shule za msingi kampuni ya kiribo Limitedi kupitia mkurugenzi wake Kebacho Monata imetoa imetoa vifaa mbalimbali katiki shule ya Msingi Nyakunguru “B”Wilayani Tarime Mkoaniu Mara yakiwemo Madaftari 1000 Tanki la Maji lenye Ujazo wa Lita 2000 Kalamu Box 2 ikiwemo na Vifaa vya Michezo vyenye jumla ya Shilingi Millioni2.5.

Katika kukabidhi vifaa hivyo mbele ya Mgeni rasmi Meneja mgodi wa North Mara Garry CheapMan ,Samwel gasaya kwa niaba ya mkurugenzi wa Kilibo limited Bw Kebacho Monotha anasema kuwa kutolewa kwa msaada huo ni moja ya kuunga juhudi za serikali katika kuboresha sekta ya elimu ususani katika shule za Msingi.
“Tumeamua kurudisha asilimia ndogo ya faida  tunayoipata kutokana na uwekezaji ndani ya Mgodi wa North Mara”alisema Gasaya.

Gasaya aliongeza kuwa mkurugenzi wa kampuni ya Kiribo ameamua kurudisha faida anayoipata kwa wananchi ili kuzidi kuleta mahusiano mema kama mwekezaji mzawa na kuweza  kutatua baadhi ya changamoto zinazowakabiri wanafunzi wa shule za msingi zinazozunguka mgodi wa dhahabu wa Nyamongo.
Meneja wa Mgodi wa Dhahabu wa Nyamongo African Barrick Gold Mine (ABG) North Mara ambaye alikuwa mgeni rasmi katika kukabidhi masaada huo anasema kuwa huo ni mfano mzuri na kuomba kuzidi kuendeleza kazi za pamoja huku akiwatakma wakandalasi   kutimiza ahadi zinazotolewa kwa wananchi ili kuendeleaza mahusiano mazuri.
“Huu ni mfano mzuri unaoonesha wawekezaji wazawa jinsi wanavyosaidia katika sekta ya elimu” alisema Garry chapman.
Kwa upande wake Mwalimu mkuu wa shule ya Nyankunguru B  Mwl Donitha Mwita alitoa shukrani kwa kampuni ya Kiribo limited pamoja na mgodi wa North Mara  kwa kuzidi kuunga juhudi za serikali katika kuboresha sekta ya Elimu.
Aaidha mwalimu huyo aliomba mgodi huo kuendelea kutoa msaada ikiwa ni pamoja na ujenzi wa nyumba za walimu pamoja na ukarabati wa madarasa kwani madarasa hayo yamechakaa sana.

“Shule yetu imetelekezwa kwa mda mrefu jaribuni kutusaidia katika kukarabati madarasa ili kuboresha madarasa”alisema Mwalimu mkuu.
Shule ya Msingi Nyakunguru B ina jumla ya wanafuzi 520 wasichana kwa wavulana nyumba za walimu4 kati ya 12 madarasa 9 kati ya 12 ambapo changamoto kubwa katika shule hiyo ni  uchakavu wa majengo na upungufu wa nyumba za walimu.
                         …….Mwisho….
Powered by Blogger.