Kipato duni chanzo cha utoro shule za Sekondari



Kipato duni chanzo cha utoro shule za Sekondari

Imebainika kuwa kipato duni kwa baadhi ya wazazi na walezi wilayani Rorya mkoani Mara ni chanzo  kikubwa cha utoro katika shule za sekondari, ikiwa ni pamoja na mwamko mdogo wa Elimu kwa wazi.
Kauli hiyo imetolewa na Mwl mkuu  Joshua John Mzori  katika shule ya sekondari Buturi Wilayani Rorya Mkoani Mara kwenye mahafari ya 16 kidato cha Nne iliyofanyika hivi karibuni shuleni hapo.

Mwalimu mkuu alisema kuwa baadhi ya wanafunzi wamekuwa wakiacha shule na kujiingiza katika sula zima la ujasiliamali ili kuweza kupata kipato cha kutunza familia.
“Baadhi ya Wazazi na walezi kipato chao ni kidogo hivyo utumia fursa hiyo kuwaruhusu wanafunzi kujiingiza katika sula la ujasiliamali na kuondokana na Masomo” alisema Mwalimu mkuu.

Zedekia Oloo Siso kwa niaba ya mgeni rasmi mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya Ya Rorya Samwel Kiboye Maarufu kama Namba Tatu aliweza kuendesha harambee  katika maafari hayo ili kuweza kuongeza nguvu katika ujenzi unaoendelea wa mahabara ambapo wazazi hawakuonesha moyo mkubwa wa kuchangia ili kuweza kuandalia wanafunzi mahalli pazuri pa kusomea.
“Kulingana  na juhudi nilizozifanya kwa kuchangisha katika maafari haya bado wazazi wameniangusha” alisema Zedekia.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi wa shule ya Sekondari Buturi iliyopo Wilayani Rorya Mkoani Mara  John Olala Kolimba alisema kuwa amekuwa mwenyekiti atangu kufunguliwa kwa shule hiyo mpaka sasa ni mwaka wa 8 amedai kuwa waliamua kujenga hosteli shuleni hapo ili kuondoa changamoto zinazo wakumba watoto wa kike na kupelekea kukatisha masomo.

Shule ya sekondari Bjuturi iliyopo Rorya mkoani Mara ina jumla ya wanafunzi 365 kwa upoande wa wahitimu walioitmu shuleni hapo ni 44 huku wasichana wakiwa 18n na  wavulana 26 na ambao walijiandikisha kufanya mtihani ni wanafunzi 48 na waliobahatika kufanya Mtihani na 44 pia shule hiyo inakumbwa na changfamoto ya ukosefu wa maji pamoja na walimu wa masomo ya sayansi.
…………………………………Mwisho……
Powered by Blogger.