Auawa kwa kuchomwa kisu kifuani
MKAZI wa
Mjini Tarime Mkoani Mara Mwita Matutu 28 ameuawa kwa kuchomwa kisu kifuani
upande wa kulia na kufa papohapo na Chacha Marwa Mapengo 30 wa Sirari.
Akizungumzia
tukio hilo kwa waandishi wa habari kamishina msaidizi wa jeshi la mpolisi mkoa
wa kipolisi Tarime/Rorya ACP Lazaro Mambosasakwa alisema kuwa tukio hilo
lilitokea majira saa 3.45 usiku wa kuamkia Novembea 19,mwaka huu.
Aidha Mambosasa
aliongeza kuwa chanzo cha kuchomwa kisu marehemu ni ugomvi uliozuka baina ya
marehemu na Chacha MWITA Mapengo Wa sirari wakati wakiwa wanakunywa pombe
katika Bar ya Chirs Pamp ya mijini hapa.
‘’Natoa wito
kwa wananchi kuacha mara moja kujihusisha na vitendo vya vurugu kama kuna
tofauti wazifikishe sehemu husika ili ziweze kushugulikiwa’’alisema Mambosasa.
Kamanda huyo
aliongeza kuwa jeshi la polisi lina mshikilia na kumhoji mtuhumiwa punde upelelezi
utakapo kamilika atafikishwa mahakamani ili kukabiliana na shitaka.
………………………………………………………..mwisho………………………………