Auawa kwa mapangaTarime
Auawa kwa mapanga Tarime
Mtu mmoja aliyejulikana kwa jina la Matiku
Makenge Ghati mwenye umri wa miaka 50
mkurya mkulima mkazi wa kitongoji cha Ngalamu kijiji Rosana kata ya Nyarerero
wilayani Tarime Mkoani Mara ameuawa kwa kutatwa mapanga sehemu za kichwani
mapanga nawatu wasiojulikana na kusanbabishiwa kupoteza maisha yake.
Kamanda wa
polisi mkoa wa kipolisi Tarime Rorya
Kamishena msaidizi wa jeshi la polisi Benedict Lazaro Mambosasa
amedhibitisha kutokea kwa tukio hilo nakusema kuwa marehemu alivamiwa Novemba
19 karibu na nyumba yake kipindi akitoka matembezini na kushambuliwa kwa
mapanga.
“Kutokana ka
tukio hilo hatujabaini mtuhumiwa yeyote
lakini badoijeshi la polisi linaendelea na uchunguzi ili kubaini wahuska na kuchulua
hatua dhidi yao” alisema kamanda.
Mambo sasa
aliongeza kuwa mwili wa marehemu umeifadhiwa katika hospitali ya mji wa Tarime
kwa ajili ya uchunguzi zaidi.
Aaidha
kamanda huyo ametoa wito kwa jamii kuwa wajijengee tabia za kutoa taarifa pale
wanapoona vitendo vya kiarifu vinatendeka ili jeshi la polisi liweze kufika
mara moja na kuwatia mikonono waharifu hao.
Sanjari na
hayo lazaro almesisitiza suala la Amani ususani tunakoelekea katika chaguzi za
serilai za mitaa.
“Tunaelekea
katika chaguzi wananchi tutunze amani na viongozi wasiingilie wananchi ili
kuwarubuni bali waache wakachague viongozi wanawapenda” alisema kamanda.
…Mwishoi…