Makambazi wawili raia wa Kenya wauawa na wananchi Tarime



Makambazi wawili raia wa Kenya wauawa na wananchi Tarime

Watu wawili wanaoaminika kuwa raia wa Kenya  wameuwa na wananchi Wilayani Tarime kwa kushukiwa kuwa ni majambazi baada ya kuhisiwa kuiba pikipiki na kuificha ndani ya nyumba anayoishi mmoja wa majambazi hao.
Tukio hilo lilitokea jana majira ya saa 12 asubuhi katika kitongoji cha Sokoni kijiji cha Sirari kata ya Sirari Wilayani hapa kwa wananchi kufanya dori katika mji wa Kebwe Lokobo 42 mwanamke aliyekuwa akiishi na mmoja wa majambazi hao kama mpenzi wake.
Kamanda wa polisi mkoa wa kipolisi Tarime Rorya kamishina msaidiozi wa polisi Lazaro Mambosasa alithibitisha kutokea kwa kutio hilo na huku waliwaawa wakitajwa kuwa ni Joel Mwita (27) mkazi wa Maabela na Samwel Mwita (25) mkazi wa Maeta wote nchini Kenya.
Miili ya marehemu hao imehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti katika Hospitali ya Wilaya ya Tarime ikisubiri familia kwa utambuzi na kwa maziko.
Mwenyekiti wa kijiji cha Sirari Nyangoko Romani alisema kuwa Oktoba 11 alipata taarifa kutoka kwa mwanakijiji wake Chacha Monanka kuwa usiku wa kuamkia siku hiyo alivamiwa na majambazi nyumbani kwake na kunyanganywa pikipiki aina ya SunLG lakini wakahisi vijana hao wawili kuhusika.
“Tuliitana kufanya doria kuanzia saa moja na nusu usiku tukazingira nyumba aliyokuwa Samwel Mwita ilipofika saa 11 alfajiri tulimgongea na  kumtoa nje  baada ya kuhojiwa alikiri na kutupeleka kwa mwenzake Joel Mwita ambapo walisema walipoificha pikipiki ile” alisema Roman na kuongeza:
“Niliwaomba wananchi wasiwashambulie kwanza ili tupate kuwahoji na kupata mtandao wote, lakini hali ilibadilika hata mimi na wenzangu tukapigwa mawe na kuamua kukimbia wananchi wakavunja mlango na kuitoa pikipiki nje na kwa kutumia magodoro na vyandarua wakawaasha moto” alisema.
Kufuatia hatua hiyo Kebwe Lokobo (42) alitoroka na kuingia kwenye gari la polisi kujisalimisha baada ya mpenzi wake kufahamika kuwa ni mwizi huku yeye akimhifadhi na vitendo vuya ujambazi kuongezeka katika eneo hilo la Sirari.
“Zaidi ya pikipiki 13 zimeporwa lakini alipohojiwa wamesema wamehusika kwenye matukio manane kwa kuiba pikipiki aina ya SunLG 3, Boxer 3 na pvs 2 zote wanaenda kuziuza rift valley nchini Kenya” alisema Mwita Rhobi.
                                                                   Mwisho.
Powered by Blogger.