Kabaka azindua kampeni za kupinga ukeketaji Tarime.

Picha ya Mama kabaka baada ya kukata utepe katika uzinduzi wa kampeni za kupinga Ukeketaji na Ndoa za Utotoni Tarime



Waziri wa kazi na ajiri Gaudensia Kabaka amezindua kampeni za kupinga Ukeketaji pamoja na ndoa za utotoni katika wilaya ya Tarime mkoani Mara.
Uzinduzi huo ambao umeambatana na sherehe za mtoto wa kike duniani ambazo uazimishwa kila mwaka Okitoba 11kwa lengo la kutetea haki ya mtoto wa kike kwani amekuwa akinyimwa haki zake za msingi kulingana na vitendo vya unyanyasaji anavyofanyiwa huku kauli mbiu ikisema kuwa kumwawezeshawasichana kumaliza kumaliza mduara wa ukatili.
Kampeni hizo kitaifa zilizinduliwa jijini Dar es salaam mnamo Agosti mwaka huu na waziri wa Maendeleo ya jamiij jinsia na watoto, Mama Graca  Machel mtetezi wan a mwanaharakati wa kutetea haki za watoto wa kike duniani.
Shere hizo ambazo zimefanyika katika viwanja vya tarafa ya Inchugu kata ya Sirari wilayani Tarime kabaka alisema kuwa jamii haina budi kukubali mabadiliko kwa lengo la kukomboa mtoto wa kike.
 Gaudensia aliongeza  kuwa kumkeketa mtoto wa kike ni moja ya chanzo cha kumuandaa katika  ndoa za utotoni kwa hali hiyo jamii inatakiwa kuondokana na mila hiyo potufu ili kumpa mtoto wa kike nafasi ya kuendelea na masomo.
’Wakati wa mababu zetu wanadhimisha saro walikuwa na maana nzuri lakini katika kipindi hiki cha kizazi kipya  mila hiyo imepitwa na wakati kwa kuzingatia kuwa kuna mchanganyiko wa makabila na nikizazi cha Dotikomu’’alisema kabaka.
Kwa upande wake mwakilishi wa  Waziri wa jinsia na watoto Sophia Simba Bernard Mwisanya alisema kuwa haki sawa ya mwanamke inayodaiwa haitapatikana kama jamii haiko tayari kuondokana na Vitendo vya ukatili dhidi ya mtoto wa kike.
Aidha Mkuu wa wilaya ya Tarime John Henjewele alizidi kuonya jamii kuondokana na kutumia nyara za serikali   bila kibali na kuwa hatua kali zitachukuliwa dhidi ya wale watakaozitumia bila kibali cha serikali.
Naye mkuu wa wilaya ya Butihama Angelina Mabura alitoa rai kwa wazazi wenye tama na mali kwa kuozesha mtoto wa kike ili waweze kubadili maisha yao kuondokana na  vitendo hivyo mara  moja.
“Watoto endeleeni kupaza sauti ukisikia  baba, Babu, Shangazi anapanga kukukeketa paza sauti tutasikia mara moja na kufanyia kazi kilio chako” alisema Mabura.
Sanjari na hayo  Mkurugenzi wa jukwaa la utu wa mtoto (CDF) Mtandao Koshuma Mtengeti alisema lengo la kufunguliwa kwa kampeni hizo ni kuendelea kuwekezesha wasichana kwa kuwajengea uwezo wawao ili kuweza kusimamia haki zao na kupaza sauti zao juu kwa mambo ambayo yanawahusu na kuweza kutoa taarifa pale haki zao zinapovunjwa .
Kauli mbiu yetu leo inasema kuwa “kupinga ukeketajina ndoa za jutotoni ni jukumu letu sote” hivyo kila mtu anayonafasi ya kumlinda mtoto wa kike ili aweze kutimiza ndoto zake.
Aidha Mtengeti alizidi kusemakuwa Jukwa la utu wa mtoto (CDF) Mtandao wataendelea na zoezi la kukuza uelewa wa wananchi juu ya madhara ya ndoa za utotoni na ukeketaji hususani wazazi na jamii kwa ujumla ili kutokomeza vitendo hivyo.
Kamanda wa polisi mkoa wa Kipolisi  Tarime Rorya  kamishena msaidizi Lazaro Mambosasa alizidi kuhasa jamii kwa ujumla kuendeleza ujasiri wa kutoa taarifa na kuongeza kuwa madawati ya jinsia yatazidi kufanya kazi kwa ufasha ili kutimiza ndoto za mtoto wa kike huku akitoa onyo kwa Ngariba watakao fanya vitendo vya ukeketaji.
“Hapa nilipo tayari nina majina ya Ngariba na baadhi wamejisalimisha kwangu tutawakamata na kuwachukulia hatua” alisema Kamanda.
Wakati huo huo mkurugenzi wa chama cha waandishi wa habari wanawake (TAMWA) Valerie Msoka alizidi kupongeza vyombo vya habari kwa mchango mkubwa walionayo katika kuibua na kuandika changamoto zinazowakumba watoto dhidi ya ukatili wa kijinsia.
“Vyombo vya habari ni chachu kubwa tuzidi kuvitumia ili kuibua zaidi changamotozilizojificna” alisema Msoka.
           
Kampeni hiyo iliyozinduliwa ili kupinga ukeketaji imelenga jamii ya Tarime kuondokana na vitendo hivyo kwani mwaka huu ni mwaka wa kukeketa na  imesimamiwa na Shirika la jukwaa la utu wa mtoto kwa ki             ushirikiana na mashirika mbalimbali kam vile Chama cha waandishi wa habari TAMWA, UNFPA, Child Marriege Free Zone  huku jeshi la Polisi Halmashauri za wilaya na Mji zikionesha ushiriki mkubwa kwa lengo la kufanikisha Zoezi hilo
                                            …..Mwisho…



Powered by Blogger.