Nyamisangura Sekondari wamwagiwa vitabu vya sayansi na kampuni ya airtel

Kaka mkuu wa shule ya Nyamisangura iliyopo wilayani Tarime Mkoani Mara akikabidhiwa vitabu na Meneja wa kampuni ya aitel mkoa wa Mara Joseph Mushi  kwa niaba ya wanafunzi  kulia kwake ni Ofisa masoko kanda ya ziwa Emmanuel Raphael




Shule ya sekondari Nyamisangura wilayani Tarime Mkoani Mara wamepata msaada wa vitabu vya masomo ya Sayansi vyenye thamani ya  zaidi ya shilingi millioni nne kutoka katika kampuni ya mtandao wa simu za aitel Tanzania kwa lengo la kuinua masomo ya sayansi katika shule za sekondari.

Katika kukabidhi msaada huo wa vitabu vya masomo ya sayansi Joseph Mushi ambaye ni meneja wa kampuni hiyo mkoa wa Mara alisema kuwa kutolewa kwa msaada huo ni kila mwaka.

“Kila mwaka kampuni yetu hutoa msaada wa vitabu kipindi hiki tumejikita katika sekta ya elimu ususani vitabu vya masomo ya sayansi kwa ajili ya kuinua masomo ya sayansi katika shule za sekondari” alisema Meneja.

Meneja mkoa aliongeza kuwa kutolewa kwa msada huo ni kwa sababu ya mchango mkubwa wa jamii katika kuchangia kampuni hiyo kupitia ununuzi wa maongezi hivyo asilimia Fulani urejeshwa kwa jamii ili kuweza kusapoti huduma za kijamii.

Naye Meneja masoko kanda ya Ziwa Emmanuel Raphael aliwataka wanafunzi hao kutunza vitabu hivyoi ikiwa ni pamoja na kuzidi kupenda masomo ya sayansi.
“Tunategemea wanganga kupitia Nyamisangura hivyo endeleni na moyo wa kupenda masomo ya Sayansi” alisema Meneja kanda.

Kwa upande wake mkuu wa shule ya Sekondari Nyamisangura Jolijo Zephania alitoa shukrani kwa niaba ya wazazi na kuzidi kuomba kampuni nyingine kujitkeza ili kuweza kutoa msaada.
“Shule bado ina mahitaji mengi kulingana na changamoto tulizozisoma mbele ya Mgeni rasmi” alisema Mkuu wa shule.

Ofisa elimu msaidizi katika Halmashauri ya Mji wa Tarimea Wegoro Mtarasha ambaye pia alikuwa mwakilishi wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Tarime Venance Mwamengo alizidi kusisitiza walnafunzi hao kuazima vitabu kwa lengo la kuvisoma

Najua wengine mutaazima vitabu hivi kwa ajili ya kutunza nyumbani kwenu azimeni kwa ajili ya kusoma alisema Ofisa elimu msaidizi
 Joseph Chacha ni kaka mkuu wa shule hiyo kwa niaba ya wanafunzi alisema kuwa watatumia vitabu hivyo kwa lengo la kujiongezea uelewa zaidi na kuzidi kuomba makampuni kuzidi kuwa na moyo wa kutoa misaada ili kusaidia serikali.
                     ……Mwisho….
Powered by Blogger.