Jamii saidieni wanaishi katika Mazingira hatarishi

Picha ya Mwanasheria wa kituo cha Center For Widows and Children Assistance (CWCA)Bw: Ostack Mligo kilichopo Mjini Musoma Mkoani Mara kipindi akiongea na mmiliki wa blog ya Cleonews tz kuhusiana na changamoto zinazowakumba katika utendaji kazi.


Jamii imetakiwa kusaidia watu wanaishi katika mazingira hatarishi kwa lengo la kuwaondolea msongo wa mawazo kwani watu hao wakati mwingine uchukua maamuzi magumu baada ya ugumu wa maisha na kutaka kujiondoa uhai wao.

Kauli hiyo ilitolewa na mwanasheria mwandamizi wa kituo kisikuwa cha serikali Center For Widows and Children Assistance (CWCA) kilichopo Mjini Musoma Mkoani kipindi akiongea na gazeti hili ofisini kwake Mara Bw: Ostack Mligo.

Aidha Mligo amesema kuwa watu wenye uwezo na kipato kikubwa cha fedha hawako tayari kusaidia jamii yenye shida wakiwemo watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi suala ambalo linazidi kuwa changamoto,

Ameongeza kuwa shirika hilo linatoa msaada wa kisheria linasaidia watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi akina mama wajane ambapo kwa sasa mabinti 94 wamefanikiwa kupelekwa vyuo vya ufundi kupitia shirika hilo.

Sanjari na hayo mwanasheria amesema kuwa serikali haina budi kuwamstari wa mbele kwa kushirikiana na Mashirika mbalimbali ili kuweza kupambana na vitendo vya ukatili vinavyoendelea nchini hapa

Hata hivyo Mwanasheria amezitaja changamoto wanazokumbana nazo kuwa ni hali ngumu ya maisha kwa watu wanaitaji huduma ya kusaidiwa kwani uhitaji fedha ili kuweza kufuatilia kesi zinazokuwa zinaendeshwa katika maeneo mbalimbali

                        ……Mwisho…


Powered by Blogger.