Wanawake wadai haki sawa

Wanaharakati wakiwa katika kongamano la TGNP Mtandao wakiwana mabango yenye ujumbe jana ni katika ofisi za Tgnp Mtandao jijini Dar es salaam.


                                          Wanawake wadai haki sawa

Wana harakati kutoka katika mikoa mbalimbali wakiungana na mtandao wa jinsia Tgnp jijini Dar es salaamu  wamehungana kwa pamoja na kupaza sauti ya pamoja ili kudai haki sawa  kupitia kongamano lililofanyika katika viwanja vya Ofisi za TGNP Mtandao jijini hapa ikiwa ni nipamoja na kuzungumzia mambo ya bunge maalumu la  kubainisha yatakayofanyika baada ya Bunge  maaalumu la katiba kumaliza  Octopber 04 Mwaka huu.
Kongamano hilo liliusisha baadhi ya waandishi wa habari kutoka mikoa kama ukiwemo mkoa wa Shinyanga, Mara na Morogoro pamoja nawanaharakatikutoka mikoa mbalimbali hapa nchini yakiwemo makundi maalumu ya watu wenye ulemavu Makundi kutoka vituo vya juhudi  na maarifa vinavyowakilisha Tgnp Mtandao katika mikoa mbalimbali.
Lilian Liundi ni kaimu mkurugenzi wa Tgnp mtandao katika kuwasilisha mada kwenye kongamano hilo alisema kuwa endapo Bunge maalumu la katiba litapitisha rasimu ya katibainayopendekezwa kwa  wingi wa kura za ndiyo za wajumbe wa Bunge hilo, Mh Rais Jakaya Mrisho kikwete atakabidhiwa rasimu hiyo na kuwa katiba inayopendekezwa
 Aidha  kaimu mkurugenzi alisema kuwa  hatua itakayofuata kwa mujibu wa sheriaya mabadiliko ya katiba ni utoaji wa elimu na uhamasishaji kwa umma juu ya maudhui yaliyomo kwenye katiba inayopendekezwa kwenye katiba inayopendekezwa na kampeni ya upigaji wa kura ya maoni.
“Sisi kama wanaharakati hatuna budi kuwa mabalozi wazuri ili kufikisha ujumbe uliokusudiwa kwa jamii ususani maeneo ya vijijinia”lisema kaimu mkurugenzi.
Tgnp Mtandao wa wanawake na katiba pamoja na Mashirika yenye kupigania haki za Watanzania wataendelea kutumia fursa zilizopo ili kufikisha ujumbe uliokusudiwa ili kuelimisha jamii na kuelewa  kuhusu katiba  inayoppendekezwa ili kusaidia wakati wa kupigia kura maoni juu yakatiba hatimaye wapige kura wakiwa na maamuzi sahii.

Licha ya hayo wanaharakati hao wamezidi kusoisitiza suala zima la 50 / 50 ili kuweza kuimarisha msingi wa wa usawa
“Tunatarajia  katika marekebisho ya katiba ya mwaka 1977 itakayotumika katika uchaguzi kwenye marekebisho asilimia ya 50/50 iwepo “walisema.
 Kwa upande wake  mwenyekiti wa  wanawake katiba Prof Ruth Meena alisema kuwa kama wanawake watazidi kupambana ili yale waliyopendekeza katika rasimu ya katiba yaweze kuwekwa na kubainisha
Alisema kuwa wanawake wamekuwa wakiwekwa pembeni pale panapotokea ushindi hivyo mwanamke hana budi kushiriki katika mapambano yeyote ili kuweza kupata haki zake za msingi
Wanawake tuweze kuunganisha nguvu ya pamoja na kuweza kupambana na matendo ya unyanyasaji yanayojitokeza dhidi ya mama na motto.
“Pia  wanawake katika kongamano hilo wametakiwa kujitokeza kogombea nafasi za ngazi  za juu kuanzia uraisi  na si kupigania nafasi za chini” walisema.
                              ………Mwisho….
Powered by Blogger.