Akina mama jitokezeni kwa wingi kujiandikisha katika dafrari la wapiga kura.

Picha aliyekuwa  Mwnyekiti  vijana Taifa John Heche kulia kwake ni Katibu wa  vijana Bavicha Tai fa Mwita Jackson katika  mkutano uliofanyika jana  kwewnye viwanaja  vya Serengeti wilayani Tarime Mkoani Mara


Akina mama wilayani Tarime mkoani ,Mara wametakiwa kujitokeza kwa wingi kujiandikisha katika daftari la kudumu la wapiga kura ili kuweza kufanya maamuzi  ya kweli katika uchaguzi ujao.
Kauli hiyo ilitolewa hivi karibuni na  Mwenyekiti wa  Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) wilaya Julius Ngoto katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja wa Serengeti Mjini Tarime Mkoani Mara.
Alisema kuwa akina mama ndo waliowengi wenye kufanya mapinduzi ya kweli hawana budi kujitokeza kwa wingi katika kujiandikisha kwa wingi ili kipindi cha kupiga kura waweze kufanya maamuzi.
Naye katibu wa Baraza la Vijana Taifa ( BAVICHA) Mwita Jackson alilaani vitendo vinavyozidi kufanywa na jeshi la polisi kwa kuonea wananchi na kusema kuwa jeshi la polisi halina budi kutafuta namna ya kuishi na jamii ili kuondoa uasama.
“Kila siku tunapiga kelele kuhusiana na mauaji ya jeshi la polisi na vijana wa Mgodini lakini bado” alisema Katibu.
Kwa upande wake aliyekuwa Mwenyekiti wa Vijana Taifa John Heche aliwasisitiza wananachi kupitia rasmu ya katiba iliyopitishwa na kufanya maamuzi yao bila kushinikizwa na kitu chochote.
“Katiba ndo kila kitu nyie wananchi mtakapoletewa rasmu kutoa maoni fanyeni maamuzi yenye kuleta mabadiliko ya Taifa ili kuweza kukomesha wale wenye nia mbaya na Nchi yetu” alisema Heche.
Hata hivyo katibu wa Chama hicho ngazi ya Wilaya Mwl Chacha Heche alisema kuwa jeshi la polisi halina budi kujitazama kwa upya na kuondokana na manyanyaso kwa wananchi.
“Tumepewa ridhaa ya kuongoza na wananchi hivyo tutazidi kupambana mpaka haki yao inapatikana” alisema Mwenyekiti John.
                            ….Mwisho….
Powered by Blogger.