Sheikh Addulhakim Mrisho soud wanasiasa vusheni nchi kwa Amani.

Picha ya Sheikh wa wilaya Abdulhakim Mrisho Soud katika msikiti wa ijumaa Bakwata akikabidhiwa msaada wa mabati kushoto kwake ni ktibu msaidizi wa Chama Cha Mapinduzi wilaya Kapis Adogo akikabidhi msaada huo wa mabati 45 yenye thamni ya shilingi laki tano na elfu tano kwa niaba ya mbunge wa jimbo laTarime Nyambari Nyangwine wengine ni vingozi wa (CCM )akiwemo katibu wazazi na mwenezi wilaya



Wanasiasa wametakiwa kuvusha nchi kwa Amani ikiwa ni pamoja na kuwa na uzalendo na nchin yao,ili kuweza kulishisha kizazi kinachokuja mambo mazuri na si kuacha machafuko kwa sababu ya uchu wa madaraka.

Kauli hiyo ilitolewa hivi karibuni katika msikiti wa ijumaa Bakwata na Sheikh wa Wilaya ya Tarime Mkoani Mara  Sheikh Abdulhakim Mrisho Soud kipindi akikabiddhiwa msaada wa mabati 45 yenye thamani ya shilingi laki tano na elfu tano.

Sheikh huyo alisema kuwa wanasiasa hawana budi kushindana kwa sera na si kushindana kwa nafsi suala ambalo linaweza kusababisha machauko ya nchi.

“Kwa sasa haya yote yanafanyika kwa sababu ya amani ya Tanzania machafuko yakianza kwa sababu ya wanasiasa kizazi kinachokuja kitajifunza nini?” alisema sheikh.

Naye katibu msaidizi wa Chama Cha Mapinuzi( CCM) Kapis Adogo kwa niaba ya mbunge wa jimbo la Tarime katika kukabidhi msaada huo alisema kuwa viongozi hawana budi kutoa msaada bila kujali itikadi ya vyama wala dini.

“Tutazidi kushiikiana na viongozi wote bila kujali itikadi ya vyama wala dini lengo kubwa ni kuleta mabadiliko katika wilaya yetu” alisema katibu msaidizi.

Kwa Upande wake katibu wa wazazi wilaya Mathias Lugola aliwataka wazazi na walezi kulea watoto wao katika maadili ya kidini ikiwa ni pamoja na kuendeleza mila za kiafika.

Kundi kubwa la vijana wamebadilika hivyo wazazi hawana budi kuzidi kuwalea katika maadili ya kidini ili kurudisha maadili alisema katibu wazazi

Naye mbunge wa jimbo la Tarime Nyambari Nyangwine aliongea na gazeti ili kwa njia ya simu kuwa msaada huo ni moja ya kutekeleza ahadi ambazo amehaidi katika uongozi wake.

“Nimekuwa nikitekeleza ahadi nyingi na huo msaada wa mabati ni moja ya kutimiza ahadi zangu kama mbunge” alisema.

Nyambari aliongeza kuwa vijana hawana budi kujishuhulisha kwa lengo la kjikwamua na si kutegemea serikali
                       ….Mwisho….
Powered by Blogger.