WAJUMBE WA KULINDA HAKI YA MTOTO WAPEWA MAFUNZO:

P
Picha ya mkufunzi ambaye ni Mwanasheria wa Halmashauri ya wilaya ya Tarime Mkoani Mara akitfafanua sheria ya Kulinda mtoto ni katika ukumbi wa Ofisi ya kata ya Sirari

WAJUMBE WA KULINDA HAKI YA MTOTO WAPEWA MAFUNZO:

Wajumbe ishirini kutoka kata ya Nyamaraga na  kata ya Sirari Wilayani Tarime mkoani Mara wmepeta mafunzo  juu ya kutambua sheria ya kumlinda mtoto ya Mwaka 2009 ikiwa ni pamoja na mafunzo juu ya kupinga ukatili wa kijinsia dhidi ya mamana mtoto.

Mafunzo hayo yamefadhiliwa na Shirika la Center For Children Assistance (CWCA)  ambapo yamefanyika leo katika ukumbi wa ofisi ya kata ya Sirari kwa kuhusisha  wajumbe wawili kutoka katika kata za  sirari na Nyamaraga,na vitongoji vilivyohusika ni Kitongoji cha Sokoni,kanisani,Mpakani,Buriba,Ngerengere,Remagwe, Kitagasembe na Gwitirio lengo ni kupata elimu  juu ya Sheria ya kumlinda mtoto ya Mwaka 2009.

Kwa Upande wake Joseph Vungwa ambaye ni Mwanasheria wa Halmashauri ya Wilaya ya Tarime  ammbaye pia amekuwa mseminishaji katika Mafunzo hayo alisema kuwa wajumbe hao hawana budi kuyafanyia kazi mafunzo watakayo yapata kwa lengo la kuleta mabadiliko ndani ya jamii.

“Lengo la Mafunzo ni kila mtu kuelewa sheria hii ya kulinda mtoto kwa lengo la kuleta mabadiliko dhidi ya mtoto” alisema Vungwa.

Stephen Ngoyani ni Mratibu wa vipindi vya kuelimisha jamii juu ya haki ya mtoto kutoka katika shirika la Center for Widows and Children Assistance (CWCA) lililopo Musoma Mjini  ambapo makao yake makuu yapo Dar es Salaam.

Ngoyani alisema kuwa Shiriki hilo linajiusisha na kutoa mafunzo  ya mtoto Na  21 ya  Mwaka 2009, Ukatili wa kingono kwa mtoto  pamoja na uendeshaji wa kesi za ukatili wa kingono kwa  mtoto katika Mahakama.
 Aliongeza kuwa shirika hilo linayo miradi mbalimbali ikiwemo ya kutoa usaidizi wa kisheria katika jamii, kutoa huduma ya kusomesha wanafunzi wanaoihi katika mazingira hatarishi lengo kubwa ni kusaidia  jamii.

Nao washiriki wa mafunzo hayo walisema kuwa mafunzo hayo yawee endelevu ikiwa ni pamoja na kufikia wahusika wote ususani maeneo ya Vijijini kwa lengo la kufikiwa walengwa

“Wahathilika wa matukio haya wengi wako vijijini hivyo tunaomba haya mashirika yakiwemo mengine wawezekufika vijijini ili kutoa huduma” walisema Wajumbe.

Mafunzo hayo yanaemndeshwa takribani siku  mbili ikiwa ni kufi ili kuweza  kuelimisha wajumbe hao kwa lengo la kuwa mabalozi kupitia vitongoji, Vijiji na  Kata

                                
Powered by Blogger.