Binti miaka 19 abakwa na wanaume wawili.
Binti miaka 19 abakwa na wanaume wawili.
Binti mmoja jina limeifadhiwa
mkazi wa Nyamikoma kijiji cha Nyangoto Wilayani Tarime MkoaniMara alibakwa na wanaume
wawaili huku akiwa ameshikiliwa na panga
pamoja na kisu na kumusababishia maumivu makali
Binti huyo alisema kuwa Watu
hao wawila akiwemo mme wake wa ndoa na kwa sasa ni takribani miaka mitano
wameachana japo hajapewa taraka walimkuta eneo la Ofisi ya serikali ya kijiji
cha nyangoto akiwa anasigina karanga za kupika ndipo walimshika kwa nguvu wakiwa na mapanga na kupelekwa
katika nyumba moja jirani na alipo kuwa akiishi hapo awali nakuanza kubakwa kwa
zamu.
“Mme wangu anayefaamika kwa
jina la Kerement Aizaki Miaka30 Mkazi wa kijiji cha kewanja Nyamongo alianza
kunibaka badaea akaingia rafiki yake sikujua jina lake wakiwa wameshika mapanga
na visu na badae rafiki yangu alienda akatoa taarifa kwa kaka yangu ndipo
alienda polisi na kuleta polisi wakanitoa ndani majira ya saa nane mchana na
akakamatwa mme wangu lakini rafiki yake alikimbia” alisema Binti huyo.
Chacha Masicho ni kaka yake
na binti aliyefanyiwa ukatili huo alisema kuwa baada ya kupata taarifa alienda
kituo cha polisi cha Nyamwaga na kutoa taarifa na ndipo polisi walielekea eneo
la tukio na kukumatwa kwa mtuhumiwa huyo.
“Kinachozidi kunishangaza ni
kwamba mtuhumiwa alipwlekwa mahakamani kwa kesi ya hapo awali kwani alishawai
kumpiga mpaka akazirai lakini kesi ya ubakaji ilitupwa na amepata dhamani sasa
tutafanyaje ili kumkamata iliataje rafiki yake” alisema Chacha.
Kaijage Kagumillwa ni mganga
mkuu wa haspitali ya sungusungu iliyopo Nyamongo alisema kuwa binti huyo
alipokelewa hospitalini hapo na kufanyiwa uchunguzi na kukutwa akiwa
amechubuliwa sehemu zake za siri lakini hakukutwa na maambukizi yeyote na kuanzishiwa
dawa za kuzuia maambukizi
Kamanda wa polisi Mkoa wa
kipolisi Tarime Rorya ACP Benedict Mambo sasa alidhibitisha kutokea kwa tukio hilo na kuzidi kulaani
vitendo hivyo ambavyo vinatendeka
….Mwisho…