JAMII YASHAULIWA KUFUGA NYUKI

JAMII YASHAULIWA KUFUGA NYUKI

Jamii imeshauliwa kufuga nyuki kwa ajili ya kujiingizia kipato ikiwa ni pamoja na kuongeza uchumi wa  nchi.

Kauli hiyo ilitolewa jana na Diwani wa kata ya Nyamaraga Wilayani Tarime Mkoani Mara Bw Antony Manga  kipindi akiongea na Wanakikundi wa kikundi  cha  Ufugaji Nyuki kinachojulikanakwa jina la Twiga Mazingira na Nyuki kilichopo kjiji cha kitagasembe kata Nyamaraga kikiwa na wanakikundi 25 walio hai.

Diwani huyo alisema kuwa jamii haina budi kuwekeza katika ufugaji wa Nyuki  kupitia Vikundi mbalimbali ya Ujasiliamali ili kuweza kujiongezea kipato pamoja na kuinua Uchumi wa Nchi.

“Mimi kama diwani nitazidi kuhamasisha jamii ili kuweza kupenda kilimo cha alizeti kwa Nyumi wanapenda maua ili waweze kutengeneza Asali” alisema Antony

Christopher Momanyi ni mkazi wa Kijiji cha Nyagisembe kata Nyamaraga na ni Mfanyabihashara katika Mji mdogo wa Sirari ambaye pia ni Mmoja wa kikundi cha Ufugaji wa nyuki alisema kuwa alianza kufuga Nyuki akiwa anajitegemea kuanzia Feburuari Mwaka jana na mpaka sasaana zaxidi ya mizinga mia na ameweza kusomesha watoto kupitia Ufugaji wa Nyuki.

“Mpaka sasa najiwekea liba ya shilingi Elfu hamsini kwa lengo la kuendeleza ufugaji huu” alisema Momanyi.

Robi Marwa ni Mwenyekiti wa kikundi hicha cha Ufugaji wa nyuki alizitaja changamoto zinazowakabili kuwa ni ukosefu wa Soko, Upungufu wa mizinga ya kisasa pamoja na vifaa vya kulinia asali

Kwa Upande wake Diwani wa kata ya Binagi  Leonard Matiko alisema kuwa ameamua kuondokana na Ufugaji wa Ngombe na Kilimo cha Kisasa kwa lengo la kuendeleza kilimo cha Ufugaji wa Nyuki

“Baada ya kuona Mifugo inashambuliwa na wezi nimeamua kuingia katika ufugaji wa Nyuki ambao hauna Changamoto japo bado tunakumbwa na changamoto za ukosefu wa soko na vifaa” alisema Diwani huyo.
                          
Powered by Blogger.