Balozi wa papa wakristo dumisheni Upendo, Mshikamano na Amani



WAKRISTO   wamewaasaa kuheshimu  na  kutunza maumbile ya miili yao ambayo ni hekalu na kuona umuhimu wake  ikiwa ni sehemu ya Uumbaji wa binadamu ili kutokwenda kinyume  na sheria ya maumbile ya Mwenyezi Mungu.


Hayo yalisemwa na Askofu Mkuu  Francisco Montecillo Padilla  Balozi wa Papa wa Vaticani nchini Tanzania wakati akizungumza na wakristo wa Parokia ya Tarime katika ibada ya  athimisho la kiekaristi Takatifu lilofanyika wilayani humo.


Padilla alisema kuwa wakristo wengi wamesahau sheria ya maumbile ya Mwenyezi Mungu kwa mwanadamu ambayo ni hekalu la Mungu na kuyaharibu pasipo kujua kuwa ni kumkosema Mungu aliyeumba maumbile hayo.

Alisema sheria hairuhusu na  wanapofanya vitendo hivyo ni chukizo mbele za Mungu na hivyo kuwaomba wawe na upendo ,amani,na mshikamano miongoni mwao na kufuata mafundisho ya Baba Matakatifu.

Aliwasihi kuacha machafuko ya  na vurugu katika makanisa ili kufanya yale yanayompendeza Mungu kwani mafundisho ya Mungu yanapenda  watu waishi kwa amani na upendo.

Aliwaomba kutumia ardhi waliyonayo vizuri kwani wamebarikiwa sana kuliko maeneo mengine ya nchi kwa kuwa  ardhi waliyonayo ina rutuba na  maliasili nzuri kwa ajili ya kujiletea maendeleo.

Wakati huohuo ulinzi mkali wa jeshi la polisi umeimarishwa kila kona ya kanisa hilo ili kuepusha mashara ambayo yanaweza kutoea katika ibada hiyo huku waumini wakitangaziwa kuzima zima na kutofanya mawasiliano ya aina yoyote mpaka mwisho wa ibada.

Askofu wa jimbo Katoliki la Musoma Michael Msonganzila aliwaeleza waumini hao kuwa lengo la ziara ya Askofu mkuu ni kuleta ujumbe wa Papa Askofu Francis wa XXVI kwa kuwaunganisha  kupitia kushiriki katika ibada ya pamoja.

Msonganzila alisema kupitia ibada wanawahamasisha waumini kuachana na mambo ya ukeketaji kwa wanawake kwa kujua madhara yanayowapata wanawake wengi hasa wakati wa kujifungua na hata maambukizi ya magojwa mengine.


Powered by Blogger.