MWILI WA ALIYEKUFA KATIKA AJALI YA BUTIAMA WAFUKULI


MWILI wa marehemu Juma Sayi  mkazi wa musoma Mkoani Mara, ulikutwa umefukuliwa kaburini katika makaburi ya Musoma Basi na watu wasiojulikana usiku wa kumkia leo.
kwa mjibu wa taarifa  za mwili huo zilizotolewa na msemaji wa familia aliyefahamika kwa jina  moja la Sayi, zlisema kuwa mwili huo ulikutwa umefukuliwa kaburini na kukutwa nje ya kaburi hilo leo asubuhi.
Kwa mjibu wa msemaji wa familia hiyo alisema kuwa baada ya watu hao wasio julikana walipomaliza kuufukua na kuuweka nje ya kaburi hilo walichukua ubao uliowekwa kaburini wakati wa mazishi hayo na kutoweka nao pasipo julikana.
Tukio hilo liligunduliwa na ndugu walipokwenda leo asubuhi makuburini hapo ikiwa ni siku ya tatu tangu marehemu huyo azikwe Jumamosi, Septemba 6 mwaka huu.
'' Tulikwenda kwenye kaburi la ndugu yetu katika makaburi ya Musoma Basi tuliko mzika kwa imani ya dini yetu ya kiislaamu na kukuta mwili wa marehemu ukiwa umefukuliwa ndani ya kaburi lake na kukuta nje kukiwa kumechukuliwa ubao tuliomzika nao na watu wasio julikana'' alisema Sayi.
Mara baada ya kukuta tukio hilo walifahamisha Jeshi la Polisi chini ya kamanda wake mkoa wa mara Phillip  Karangi lililofika na kuthibitisha tukio hilo leo.
Mwili huo ulirejea kuzikwa tena makaburini hapo katika kaburi hilo baada ya kumalizika kufanyika uchunguzi wa daktari na kukutwa ukiwa salama.

Tukio hilo limedaiwa na baadhi ya watu kuhusishwa na imani ya kishirikina kwa ,kile kilichodaiwa kuwa sio kawaida marehemu mwili wake uzikwe na kisha kufukuliwa bila utaratibu unaofahamika.
'' Sio kawaida mwili wa marehemu kama huyu Juma Sayi, tuliyemzika hapa na baada ya siku tatu ya leo tunakuta umefukuliwa na kuchukuliwa ubao tuliomziika nao kaburini wanaupelekea wapi na ni kwanini waufukuwe kama sio wachawi wanaokwennda kufanya mambo yao ya kishirkina?'',alihoji mmoja wa wanandugu
Marehemu Juma Sayi alifariki dunia katika ajali ya gari iliyotokea eneo la sabasaba [Songora] kitongoji cha Irimba katika mto Rwako wilaya ya Butiama  hivi septemba 5, mwaka huu asubuhi iliyohusisha magari matatu, ya J4 EXPRESS  ya aina ya YU TONG ya usajaili T 677 CYC lilipogongana uso kwa uso na gari la MWANZA COACH aina ya SCANIA la usajili  T 368 AWJ.
Ajali hiyo ilitokea baada ya kugongwa gari dogo la aina ya TOYOTA la usajaili  T 332 AKK  na basi la J4 EXPRESS lililotokea Mwanza kuelekea Sirari [Tarime] na kuanguka chini ya daraja hilo majini wakati gari la Mwanza Coach lilitokea Musoma lililoelekea Mwanza.
Katika ajali hiyo watu takribani 36 walifariki dunia papo hapo na kujeruhiwa watu 79 waliopatwa na majereha sehemu mbali mbali za mwili wake.
-----------------------------------mwisho----------
Powered by Blogger.