Wakina mama watakiwa kuwa na maamuzi ya dhati

Picha ya mbunge wa viti maalumu jimbo la Tarime Ester Matiko akiongea na waandishi wa habari pamoja na wananchi mbele ya ofisi za chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)baada ya kuchaguliwa  kuwa Mwenyekiti wa akina Mama Mkoa wa Mara katika chaguzi zilizokuwa zikifanyika Musoma mkoani Mara ili kupata viongozi katika ngazi mbalimbali kulia kwake ni katibu wa mkoa wa Mara aliyechaguliwa katika chaguzi hizo Mwl Chacha Heche.


Wakina mama wametakiwa kuwa na maamuzi ya dhati katika nyakati za uchaguzi ili kuweza kuwapata viongozi waadilifu na wa kuleta mabadiliko katika jamii.

Kauli hiyo ilitolewa jana na Mbune wa viti maalumu kupitia tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Bi: Ester Matiko kipindi akiongea na gazeti ili baada ya ushindi wa kuwania kiti cha mwenyekiti wa akina mama mkoa wa Mara katika chaguzi zilizokuwa zikifanyika hapo juzi mjini musoma mkoani Mara ili kuweza kuwapata viongozi katika nyadhifa mbalimbali kupitia ngazi ya Mkoa.

Mbunge alisema kuwa wanawake hao hawana budi kuondokana na zawadi ndogondogo  zinazotolewa na wagombea katika nyanja mbalimbali bali waunganishe nguvu ya pamoja ili kuweza kujikwamua na kufanya mapinduzi katika uongozi.

“ Nimechaguliwa kuwa Mwenyekiti wa akina mama mkoa wa Mara hivyo naitaji nguvu kubwa na ushirikiano kwa akina mama ili tuweze kujikwamua” alisema  mbunge.

Aidha mbune huyo alisema kuwa atatumia fursa aliyonayo kuwahamasisha wakina mama ili kujiunga na vikundi huku wakianzisha ujasiliamali kwa lengo la kujikwamua katika uchumi.

“Wanatarime ni wakati maalumu kushirikiana na viongozi ili kuweza kufanya mapinduzi na kujenga jimbo letu  huku tukikemea makundi  yanayoanzishwa hapa”  alisema.

Kwa upande wake katibu wa chama hicho Mwl Chacha Heche alisema kuwa katika utendaji wake wa kazi ataweza kushirkisha viongozi wote wazee ili kuweza kushauri chama hicho na kuondoa tofauti ndani ya wilaya zote zilizopo ndani ya mkoa wa Mara.

Hata hivyo  katibu aliongeza kuwa makundi hayatakifikisha popote chama hicho bali vionozi wote waunganishe nguvu ya pamoja ili kuweza kukitangaza chama hicho upya wilayani Tarime.

Nia tunayo sisi bado ni wazalendo nia yetu ni kusikiliza wananchi na kufanya mambo ya maendeleo alisema katibu huyo.
                                …..Mwisho….

Powered by Blogger.