Kopa kokakola wachagua vipaji Tarime.



Kopa kokakola wachagua vipaji Tarime.

WACHEZAJI ambao walishiriki  Ligi ya Kopa kokakola Wilayani Tarime Mkoani Mara juzi  katika viwanja vya Sereneti mjini Tarime wamlitimua vumbi ili kuwasaka vijana wenye vipaji kwa lengo la kuunda timu ya mkoa hadi Taifa.

Wachezaji hao  wametoka katika timu mbalimbali zilizopo ndani ya wilaya ikiwamo timu ya mpira wa miguu Buhemba Kids,Rebu shule ya msingi,Sirari Kids,Tarime Kids,Mafundi KidsTarime United pamoja na Tadea Kids walijikuta amabapo wamejikuta wakimaliza mchuano huo kwa mazingira magumu bila chakula na badala yake wameambulia kushindia maji ya kama chakula cha mchana kwani mechi hizo zilianza majira ya asubuhi msaada huo ulitolewa na na Mbunge wa viti maalumu kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Estar Matiko
Ligi hiyo ilianzishwa na Shirikisho la Mpira Duniani FIFA chini ya udhamini wa kopa kokakola kwa lengo la kuibua vipaji.

Akizungumza juzi Kocha wa Mkoa Mara James George juu ya mchuano huo alisema kuwa kanuni za kopa kokakola ni kunyanyua soka na kusaka vipaji.

‘’Lengo ni kuwapata wachezaji 20 kutoka Wilaya Tarime ambao watakwenda kuunda Timu ya Mkoa 20 kanda na hatimaye timu ya Taifa na hapa hatuhitaji mshindi badala yake tunasaka wenye vipaji na kuteneneza safu nzuri’’alisema George.

Aidha aliwataja waliochaguliwa kwenda kuunda Timu ya Mkoa kuwa ni paja na Willbardi Pastori,Ayubu Joseph,Justin Morisi,Charles Chacha kutoka timu ya Rebu,Makori Baraka,Maambo Wanzagi Bonfasi Clofas wote kutoka Buhemba Kids,Mokami Issa,Joseph Chacha kutoka Sirari.

Wengine ni pamoja na Maiko Selevestar Erick Eriuta,Charles Thobias,Hashimu WatororoMwita Kisyeri,Yahaya Forouk,Dishoni Chomete wakutoka Mafundi na Omari Anderea TevienMatacha wa Tarikme United kukamilishan idadi ya wachezaji 20 kutoka Tarime kuwakilisha Mkoa.

Kwa upande wake Moja wa wajumbe wa kamati tendaji Gabriel Gweso Nyagesagane alisema kuwa Timu nyingi hazikushiriki lii hiyo kutokana na mazinira magumu ya kufika eneo la tukio sanjari na ukosefu wa usafiri.

Aidha Nyaesagane aliongeza kuwa wachezaji wamekoswa chakula kutokana na mdhamini kushindwa kuwaandalia wachezaji bajeti ambayo inakidhi mahitaji.

Aidha timu ya wachezaji wengine wameshindwa kuhudhuria kushiriki ligi ya kopa kokakola kutokana na nauli,vifaa vya michezo na mahitaji mengine ambapo mfadhili anatakiwa kutoa kabla katika viongozi wa chama cha mpira kila Wilaya.   
,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,mwisho,,,,,,,,,,,,,

  
Powered by Blogger.