Madiwani tumieni vizuri fedha kukamilisha miradi




Madiwani wilayani Tarime mkoani Mara wametakiwa kutumia vizuri fedha za miradi mbalimbali  ili kuweza kukamilisha miradi huska kwa lengo la kusukuma gurudumu la maendeleo katika kata.

Kauli hyo ilitolewa  jana na mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Tarime amabaye pia ni diwani wa kata ya Sirari Amos Sagara katika balaza la kawaida la madiwani lililofanyika katika  ukumbi wa Halmashauri hiyo.

Mwenyekiti alisema kuwa madiwani hao hawana budi kutumia fedha hizo katika miradi huska ili iweze kumalizika haraka  miradi huyo na kuondoa migogoro inayojitokeza baada ya miradi kutomalizika kwa muda mwafaka.

“Tukianza na fedha ambazo tulipewa na mgodi wa dhahabu wa African Barrick Gold Mine (ABG) uliopo Nyamongo wilayni Tarime Mkoani Mara dola laki nane na kutenga kila kata shilingi Millioni30 kwa kila kata hivyo madiwani walichagua miradi ambayo itatekelezwa sasa tumieni fedha hizo vizuri” alisema Mwenyekiti.

Hata hivyo Sagara alisema kuwa kupitia halmshauri hiyo walitoa kipaumbele suala la Afya na Elimu katika fedha hizo ambazo ziligawiwa na badae madiwani walirudi na kuomba miradi mingine kama vile barabara.

“Kulingana na miradi ambayo mmeomba nyie Madiwa itimizeni kwa wakati” alisema.

Sanjari na hayo mwenyekiti amekemea baadhi ya wakandalasi wanapata tenda za Halmashauri ya Wilaya ya Tarime na kutozikamilisha kwa muda mwafaka.

Madiwani kupitia baraza ili pitisheni ili watu kama hao wakirudi wasipate kwa sasa wanachelewesha maendeleoya wananchi alisema.


                               …..Mwisho….
Powered by Blogger.