Shule ya msingi Michire yakumbwa na uhaba wa madawati na Vyoo.

Picha ya Mbunge wa viti maalumu Estre Matiko kulia akihesabu fedha shilingi laki tano kwa ajili ya kumkabidhi diwani wa katoa ya Mukoma Kitori lazaro kwa ajili ya ujenzi wa choo katika shule ya msingi Michiri iliyopo wilayani Rorya Mkoani Mara

Shule ya Msingi Michire iliyopo Rorya Mkoani Mara inakumbwa na uhaba wa madawati na vyoo suala ambalo linapelekea wanafunzi 46 kutumia Madawati 9 katika darasa moja shuleni hapo.

Mwalimu mkuu msaidizi katika shule hiyo Mwl Elias Masatu alisema kuwa shule hiyo inakumbwa na changamoto hiyo ya uhaba wa madawati, Vyoo poamoja na  Nyumba za walimu.

“Shule yangu inajumla ya wanafunzi 373 ina matundu ya vyoo 12 wasichana Matundu 6na wavulana 6 lakini tunaekea kipindi cha mvua vitajaa na kupelekea shule kufungwa” alisema.

Sanjari na ukosefu wa nyumba za walimu zipo baadhi ya nyumba ambazo kwa sasa zina zaidi ya miaka 20 hazijakamilika kwa sababu ya migongano ya vyama vya kisiasa sula ambalo linarudisha maendeleo ya wananchi katika kata hiyo.


Kwa upande wake Diwani wa kata ya Mukoma wilayni humo Kitori lazaro alisema kuwa uhaba wa madawati katika shule hiyo ni chanamotokubwa sana.

“Katika wilaya yetu tunajumla ya shule 119 na uhaba wa madawati 9720 suala ambalo linapelekea  asilimia kubwa ya wanafunzi katika shule za msingi kukaa chini” alisema diwani huyo.

Naye Mbunge wa viti maalumu kupitia tiketi ya chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Jimbo la Tarime Bi:Ester Matiko alitoa shilingi laki tano kwa lengo la kuchangia ujenzi wa choo unaoendelea shuleni hapo.

“Mwaka jana nilialikwa kuja kuwa mgeni rasmi lakini sikupata nafasi ya  kufika hivyo sasa natoa hizi fedha kama mama mzazi ili kunusuru watoto wetu waendelee na masomo shule isifunwa kwa sababu ya choo” alisema.

Hata hivyo Katibu wa chama hicho Mkoa wa Mara Mwl Chacha Heche alisema kuwa ni moja ya kuanzi katika utendaji kazi wake na kuwataka viongozi kuonesha kazi kwa vitendo na kuondoa tofauti za vyama ili kusukuma urudumu la Maendeleo ndani ya Mkoa wa Mara.

“Lengo kubwa ni kuwa na Maendeleo ndani ya mkoa wa Mara na si kukaa ,makundi kujadili itikadi za vyama haimusaidii mwananchi wa kawaida” alisema katibu wa mkoa
                                           …..Mwisho….

Powered by Blogger.